HABARI KWA WAKATI KUTOKA HAPA

Tunakuhakikishia kupata habari zote zilizo muhimu kutoka ulimwenguni kote kwa wakati, unaweza kusubscribe mtandao wetu na ukawa unapokea habari zote katika email yako punde tu tuchapishapo machapisho yetu. Jiunge na mitandao yetu ya Facebook na Twitter kutupata kirahisi.

HABARI ZA MICHEZO

Sasa Fichuo tunakuhakikishia kupata taarifa zote za kimichezo kutoka viwanja mbalimbali duniani, lengo ni kuhakikisha hupitwi na lolote katika ulimwengu wa michezo.Jiunge na mitandao yetu ya Facebook na Twitter kutupata kirahisi.

TAARIFA ZA BURUDANI NA HABARI ZA WASANII

Unapenda masuala ya burudani? Ni jukumu letu kuhakikisha unazipata info zote za burudani na wasanii wanaokupa burudani, unapata video mpya, movie pamoja na muziki. Kaa karibu nasi.

KURASA ZA MAGAZETI KILA SIKU

Tunakupatia kila ambacho kinaandikwa katika magazeti ya Tanzania na nje ya Tanzania, usitie shaka ukishindwa kununua gazeti uipendalo, sogea karibu nasi na upate kila unachokihitaji.

MAHUSIANO

Fahamu mambo mengi katika ulimwengu wa mapenzi kwa kupitia dondoo, simulizi na visa mbalimbali kupitia Fichuo Online, Jiunge na mitandao yetu ya Facebook na Twitter kutupata kirahisi.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo AFYA. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo AFYA. Onyesha machapisho yote

Jumanne, Februari 27, 2018

UNAAMBIWA KUOGELEA BAHARINI KUNASABABISHA MAGONJWA!!!

Kuogelea baharini kunaongeza kwa kiwango kikubwa kuwa na matatizo ya tumbo , kuumwa na masikio na magonjwa mengine , watafiti wamebaini.
Chuo kikuu cha matibabu cha Exeter na kituo cha Ekolojia na maji ardhini kilifanya utafiti huo.
Ulibaini kwamba uwezo wa muogeleaji wa baharini kuwa na tatizo la masikio uko juu ikilinganishwa na waogeleaji wa maeneo mengine huku matatizo ya tumbo pia yakipanda hadi asilimia 29.

Mbali na kuogelea, hatari hizo pia zinashirikisha michezo ya baharini kama vile kuteleza kwa ubao katika mawimbi.
Watafiti waliangazia tafiti 19 zinazohusiana na uogeleaji wa baharini na magonjwa kutoka Uingereza , Marekani, Australia, New Zealnd , Denmark na Norway.
Watachanganua matokeo kutoka kwa zaidi ya watu 120,000.
''Katika mataifa yalio na wafanyikazi wenye mapato makubwa kama vile Uingereza, kuna dhana kwamba hatari za kuogelea baharini ni chache mno'', alisema Dkt Anne Leonard.Hatahivyo magazeti yetu yanaonyesha kuwa kuogelea baharini hakuongezi uwezekano wa kuugua, kama vile kuumwa na masikio mbali na matatizo yanayohusisha tumbo kama vile kuumwa na tumbo na kuendesha.
Tunadhani kwamba hii inamaanisha kwamba uchafuzi wa mazingira bado ni swala tete linalowaathiri waogeleaji katika mataifa tajiri duniani.
Mtafiti mshauri Dkt. Will Gaze alisema: Hatutaki kuwazuia watu kwenda baharini, swala ambalo lina manufaa mengi ya kiafya kama vile kuimarisha maungo.Hatahivyo ni muhimu kwamba watu wanajua athari zake ili waweze kufanya uamuzi.
Dkt Gaze amesema kwamba watu wengi hupona magonjwa hayo bila kupata tiba yoyote lakini yanaweza kuwa mabaya kwa watu wasio na kinga nzuri kama vile watu wazee na watoto.
Aliongezea: Tumetoka mbali sana katika kusafisha maji yetu, lakini ushahidi tulionao unaonyesha kuna kazi kubwa ya kufanywa.Tunatumai utafiti huu utachangia juhudu zaidi kusafisha pwani zetu.

BBC

Jumatano, Februari 21, 2018

UNASUMBUKA NA HANGOVER? TUMIA NJIA HII KUIMALIZA. TIBA!!!

Inawezekana wewe ni kati ya watu wanaopenda kupiga vyombo (Pombe) kwa kiasi kikubwa, inawezekana ni starehe yako lakini unakerwa sana na hali unayoamka nayo asubuhi, hangover, wengine kwa kiswahili kisicho rasmi sana wanaita mnng'inio na umekuwa ukipata taabu sana kuimaliza hiyo hali pengine kwa kunywa mchemsho au kutoa lock angalau kwa kunywa tena pombe kidogo.
Pamoja na njia zote uzitumiazo kumaliza hiyo hali ya mning'inio, Fichuo leo inakupatia tiba halisi, rahisi na ya asili ya kukuondolea hangover.
Kuna mchanganyiko wa kinywaji-lishe unaitwa BANANA MILKSHAKE, hiki ni kinywaji-lishe kinachotengenezwa kwa mchanganyiko wa maziwa fresh, ndizi mbivu pamoja na asali. Ukipata kinywaji-lishe hiki angalau kikombe/glasi moja katika asubuhi uliyoamka na hangover itaamsha nguvu zako na kutoa uchovu unaokupatia usumbufu.
Kwanini hii ni tiba? Kwakuwa ndizi mbivu husaidia kutuliza tumbo na kumaliza kilevi lichosalia mwilini wakati asali kazi yake ni kusawazisha na kujenga viwango vya sukari iliyoharibika mwilini.
Maziwa yenyewe tunafahamu kwamba yana vitamins zenye msaada mkubwa katika mwili wa binadamu, ambazo ni A, D, E na K

BANANA MILKSHAKE inatengenezwaje? Jifunze hapa;

Katika kutengeneza BANANA MILKSHAKE utahitaji kuwa na maziwa mabichi angalau lita moja, ndizi mbivu kubwa 2 au ndizi kisukari 4 (ndizi mbivu ndogondogo) na asali angalau vijiko vitatu vya chai. (japo hapa pia inategemeana na kiasi cha uzito na ladha uitakayo katika kinywaji-lishe chako.
Chemsha maziwa vizuri kisha wacha yapoe kabisa, kisha yatie katika brenda na uchanganye na ndizi pamoja na asali na ukoroge pamoja. baada ya hapo unaweza kutia katika friji ili upate kiwango cha ubaridi utakaoutaka haraka. Baada ya hapo inakuwa tayari kwa matumizi. Ikikusaidia saidi na wengine kama Fichuo ilivyokusaidia.

Burudika kidogo na wimbo Hangover toka kwa PSY na SNOOP

Jumanne, Oktoba 10, 2017

UNAIJUA HATARI YA KUVAA VIATU VYAKO BILA SOKSI??

Ukivalia viatu vyako bila soksi unajiweka katika hatari ya makubwa zaidi kuliko kunuka kwa miguu pekee.
Chuo cha tiba ya miguu nchini Uingereza kinasema karibuni kumekuwa na ongezeko la maambukizi ya maradhi yanayosababishwa na kuvu kutokana na kuvuma kwa mtindo wa kuvalia viatu bila soksi, hasa miongoni mwa vijana.
Mtaalamu Emma Stephenson anasema amekuwa akipokea wanaume wa kati ya miaka 18-25 walio na matatizo kwenye miguu yao ambayo yametokana na kutovalia soksi au kuvalia viatu visivyowatosha vyema.
Kutovalia soksi siku hivi kumekuwa mtindo maarufu wa mavazi, na mwanamuziki Sam Smith ni miongoni mwa watu wanaojitokeza hadharani wakiwa na viatu bila soksi.
Wanaume wengi katika maonesho ya mitindo pia mara nyingi huonesha mavazi wakiwa na viatu bila soksi.
Mwanamuziki Tinie Tempah amejishindia tuzo nyingi kwa sababu ya mitindo na mara nyingi katika maonesho ya mitindo ya Londo huketi viti vya mbele.
Yeye pia huwa mara nyingi havai soksi - lakini anafahamu madhara yake?
"Miguu ya binadamu kwa kawaida hutoa nusu painti (ambayo ni sawa na lita 0.28) ya jasho kila siku," Emma Stephenson anasema.
"Unyevu mwingi na joto unaweza kusababisha maambukizi ya maradhi yanayotokana na kuvu mfano ugonjwa unaosababisha mwasho na kuchubuka kwa ngozi (kwa Kiingereza athlete's foot)."
Kwa mujibu wa Emma, madhara yake yanaweza kuwa mabaya.
"Moja ya visa vibaya nilivyowahi kukumbana navyo ni cha mwanamume mmoja wa miaka 19 aliyefanya kazi ya kuosha magari. Miguu yake ilikuwa inatokwa na jasho sana na ilikuwa imechubuka sana."
Lakini bila shaka itachukua ujasiri kumwambia bingwa wa UFC Conor McGregor kwamba anaweza kupata matatizo kutokana na mtindo wake wa kuvalia viatu.
Emma anashauri kwamba siri ni kutozidisha, iwapo bado utataka kutovalia soksi.
Jaribu usivae viatu bila soksi kwa muda mrefu.
Jaribu pia kuweka kitu cha kukausha jasho kwenye soli ya kiatu chako kabla ya kukivalia bila soksi.
Kadhalika, kuwa makini kuchunguza miguu yako. Ukigundua unaumwa pahali tafuta usaidizi upesi.

Jumatatu, Septemba 04, 2017

TEKNOLOJIA IMESONGA, HIKI NI KIWANDA KINACHOZALISHA MBOGA USIZOHITAJI KUZIOSHA KABLA YA KUPIKWA



Kiwanda cha mimea cha idara ya utafiti wa mimea ya taasisi ya sayansi ya China chenye ukubwa wa hekta 20 kilizinduliwa mwezi Juni mwaka jana mjini Quanzhou, mkoani Fujian, China.
Katika banda la kilimo lisilo na vumbi na vijidudu, mboga mbalimbali zinakua kwenye rafu bila udongo na mwanga wa jua. Wafanyakazi wanadhibiti joto, unyevu, mwanga wa taa za LED, hewa ya Carbon Dioxide na mbolea kupitia kompyuta. Tatizo la ukuaji wa mimea kutegemea majira na hali ya hewa limetatuliwa, na mboga zinaweza kuzalishwa kiwandani kwa mfululizo mwaka mzima.
Wafanyakazi wanapoingia kwenye banda la kilimo, wanatakiwa kujisafisha mara nyingi, kuvaa nguo mbili za kikazi, barakoa na glavu, ili kuzuia vijidudu na wadudu kuingia ndani ya banda hilo. Hivyo mboga hizi hazijawahi kumwagiliwa dawa za kuwaua wadudu hata kidogo.
Mkurugenzi wa kiwanda hiki Bw. Pei Kequan alisema mboga hizi hazina hata haja ya kusafishwa kabla ya kupikwa, kwani mazingira ya kiwandani ni safi zaidi kuliko maji ya bomba.
Hivi sasa kiwanda hiki kinaweza kuzalisha tani 1.5 za mboga zisizo na uchafuzi kwa siku, na mboga hizi zimeuzwa katika miji mbalimbali mkoani Fujian.

Jumanne, Agosti 08, 2017

KUNG'ARISHA MENO NI HATARI KWA UIMARA WA MENO YAKO

Watu wengi wanatamani kuwa na meno meupe yenye kung'ara sana kwaajili ya kuboresha urembo au utanashati wao, hapa hutumika njia nyingi kuyasafisha hayo meno hata kwa njia zisizo salama.
Ni kweli tabasamu linanoga zaidi pale unapokuwa na meno safi, na wengi huamini meno ya njano huwa ni machafu hata kama yameswakiwa, na wengi wao huyachukia meno ya aina hiyo.
Ziko sababu nyingi hupelekea mtu kuwa na meno ya njano, mfano wenzangu wa Kilimanjaro wao meno yao huwa njano kutokana na aina ya maji watumiayo, lakini pia uvutaji sigara, ugoro, aina fulani za pombe na hata kutoyasafisha mara kwa mara.
Sasa wataalamu wanasemaje? Kitaalamu unaambiwa rangi halisi ya meno ni njano na si nyeupe angavu, pia tunaapiwa wale wenye kuyatakatisha meno yao na kuondoa rangi halisi pia huondoa uimara wa meno yenyewe. Muhimu ni kuendelea kuyasafisha kwa mswaki na dawa zinazoshauriwa na wataalamu wa kinywa pasipo kulazimisha kubadili rangi na kuwa angavu ili uendelee kulinda meno yako.
Leo umefahamu kuhusu hili kupitia Fichuo, karibu wakati mwingine ufahamu mengine zaidi.

Jumapili, Mei 14, 2017

KIPINDUPINDU CHAUA 115 KWA SIKU 17 YEMEN

Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu imesema mlipuko wa kipindupindu nchini Yemen umesababisha vifo vya watu 115 hususan watoto wadogo katika kipindi cha siku 17 zilizopita.
Akihutubia waandishi wa habari katika mji mkuu wa Yemen, Sana'a jana Jumapili, Dominik Stillhart, Mkurugenzi wa Operesheni wa Msalaba Mwekundu amesema vifo hivyo vilitokea kati ya Aprili 27 na Mei 13.
Afisa huyo wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu ameongeza kuwa, kesi 8,500 za ugonjwa huo zimeripotiwa kufikia sasa katika majimbo 14 ya nchi hiyo maskini ya Kiarabu.
Wakati huo huo, Sherine Varkey, Naibu Mwakilishi wa Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF nchini Yemen amesema hospitali chache zilizosalia zimeshindwa kumudu idadi kubwa ya wagonjwa na kwamba wagonjwa wengi katika Hospitali ya Sabeen katika mji mkuu Sana'a wamelala sakafuni kutokana na uhaba wa vitanda.
Mashambulizi ya kila uchao ya Saudia yamesababisha huduma za afya na matibabu nchini Yemen kukumbwa na mgogoro mkubwa.
Kuendelea mashambulizi hayo ya anga ya Saudia na waitifaki wake katika miundombinu, mahospitali, shule na makazi ya raia na kadhalika mzingiro wa kila upande wa nchi hiyo vamizi dhidi ya Yemen, kumepelekea kuenea kwa kasi maradhi kama vile kipindupindu na magonjwa mengine yanayoteketeza maisha ya wananchi wa Yemen hususan watoto.

MANUSURA WATATU WA AJALI YA LUCKY VINCENT WAPELEKWA MAREKANI

Ndege kubwa inayoweza kutumika kama ‘AMBULANCE‘ angani na iliyotoka North Carolina, Marekani kuja moja kwa moja Kilimanjaro, Tanzania kuwachukua majeruhi imeondoka asubuhi ya leo Uwanja wa KIA, Kilimanjaro.
Ndege hiyo ya Samaritan’s Purse DC 8 N782SP imewasili Kilimanjaro Tanzania jana Mei 13, 2017 ikiwa na marubani wanne na wahudumu saba tayari kuwabeba majeruhi hao ambao wataambatana na wazazi wao mpaka Marekani kwa matibabu.
Rubani wa ndege hiyo, amewaambia waandishi wa habari kwenye Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro (KIA) kwamba baada ya kuondoka, watasimama Cape Verde kuweka mafuta kisha kuelekea Marekani moja kwa moja na wanatarajia kuingia kesho.
Ndege hii imetolewa na shirika la SAMARITAN’S PURSE linalosimamiwa na mtoto wa mwinjilisti mkubwa wa Marekani, Franklin Graham, familia yao baada ya kupelekewa habari za kilichotokea kwenye ajali ya Karatu walikubali kuituma ndege hiyo kutoka Marekani kuja kuwachukua majeruhi Tanzania.
Ndege hiyo imeondoka Mei 14, majira ya mchana ikiwa imewabeba watoto hao watatu na mama zao, nesi mmoja na daktari mmoja wa Kitanzania ambao wataendelea kuwahudumia watoto hao ndani ya ndege hiyo yenye uwezo wa kutoa huduma kama ambulance pia.
Ndege hiyo ikishatua North Carolina, SAMARITAN’S PURSE wameandaa ndege nyingine ambayo pia inaweza kufanya kazi kama AMBULANCE na kuwachukua hadi Jimbo la Iowa ambako Hospitali ya Mercy imekubali kuwatibu wagonjwa hao bure kwa muda wote watakaohitaji matibabu.

Ijumaa, Mei 12, 2017

EBOLA YATINGA JAMHURI YA DEMOKRASIA YA CONGO

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kwamba ugonjwa wa Ebola umezuka katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Msemaji wa WHO nchini humo Eugene Kabambie amesema shirika hilo limechukua hatua hiyo baada ya watu watatu kufariki wakishukiwa kuwa na Ebola eneo hilo tangu Aprili 22.
WHO imesema mlipuko huo unaathiri maeneo ya msituni ya Aketi, katika mkoa wa Bas-Uele karibu na mpaka wa nchi hiyo na Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Shirika hilo limesema Waziri wa Afya wa DR Congo Oly Kalenga kupitia barua, alisema kulikuwa na watu tisa kutoka eneo la kiafya la Likati, Aketi waliohofiwa kuwa na Ebola.
Watano kati yao walipimwa na mmoja wao akathibitishwa kuwa na virusi hivyo.
Watatu kati ya tisa hao walifariki. Waziri huyo alikuwa ameiandikia WHO barua akiomba usaidizi katika kudhibiti ugonjwa huo.
"Ni kisa kilichotokea eneo lililo mbali sana, lenye msitu mkubwa, kwa hivyo tulikuwa na bahati kiasi. Huwa twachukulia kwa uzito sana visa kama hivi," alisema Kabambie.Eneo hilo linapatikana kilomita 1,300 kaskazini mashariki mwa mji mkuu wa DR Congo, Kinshasa. Kitovu cha mlipuko wa sasa ni eneo la Nambwa.
Mwaka 2014, mkurupuko wa ugonjwa huo Congo ulidhibitiwa kwa haraka ingawa watu 49 walifariki.
Watu zaidi ya 11,000 walifariki kutokana na mkurupuko wa Ebola Afrika Magharibi 2014-2015, sana nchini Guinea, Sierra Leone na Liberia katika mlipuko wa Ebola ulioatajwa kuwa mbaya zaidi kuwahi kutokea duniani. Mlipuko huo wa sasa ni wa nane kutokea nchini DR Congo tangu mwaka 1976.

Jumanne, Aprili 04, 2017

ALICHOZUNGUMZA MTOTO BRADLEY LOWREY KUHUSU KIFO CHAKE NA JERMAINE DEFOE

Mtoto Bradley Lowrey ambaye anaumwa ugonjwa wa kansa unaojulikana kama Neuroblastoma ambaye madaktari bingwa wa ugonjwa wa kansa duniani walimtabiria kuwa hakuwa na siku nyingi za kusihi, amenukuliwa akisema kuwa kila anapojisikia kuumwa sana na kudhani kuwa anakaribia kufa kama alivyoambiwa na madaktari, anakumbuka maneno ya rafiki yake mkubwa Jermaine Defoe akisema:
“Bradley, huwezi kufa kwa ajili ya kuumwa, na endapo utakufa itakuwa ni kwa amri ya Mungu na utakuwa katika mikono salama."

Jumatano, Machi 29, 2017

MKOA WA RUVUMA NA MKAKATI MPYA WA KUPAMBANA NA MALARIA

MKOA wa Ruvuma kupitia mradi wa USAID Boresha Afya umelenga kuweka mikakati ya kumaliza ugonjwa wa malaria ambao ni mkubwa katika mkoa huo, ikilinganisha na kiwango cha kitaifa, hatua itakayowezesha kupungua kwa vifo vinavyotokana na ugonjwa huo.
Mkuu wa Mkoa huo, Dk Binilith Mahenge alisema kulingana na takwimu za kitaifa, katika mkoa wa Ruvuma wajawazito wanaopata kinga ya kwanza dhidi ya malaria (IPTp-1) ni asilimia 40 na inazidi kupungua hadi kufikia asilimia saba kwa wanaopata dozi ya kinga ya tatu (IPTp-3).
Dk Mahenge alitoa kauli hiyo wakati akifungua kikao cha kutambulisha Mradi wa USAID Boresha Afya kwa mkoa wa Ruvuma kilichofanyika katika Manispaa ya Songea.
Kwa mujibu wake, hata kiwango cha malaria kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano ni asilimia 23 ilhali kitaifa ni asilimia 14 huku asilimia 39 ya kaya katika mkoa huo zinamiliki angalau chandarua kimoja na takwimu za kitaifa ni asilimia 54 na kuufanya mkoa huo kuwa miongoni mwa mikoa yenye kiwango cha chini nchini.
Alisema uzinduaji wa mpango huo ni faraja kubwa kwa serikali ya mkoa na wananchi kwa kuwa umelenga kutoa huduma shirikishi na endelevu kwa kufanya kazi na timu ya uendelezaji na usimamizi wa huduma za afya ya mkoa, halmashauri za wilaya na miji pamoja na asasi za kiraia zinazotekeleza afua za afya ngazi za jamii.
Dk Mahenge alivitaja vipaumbele vitakavyotekelezwa kuwa ni uhamasishaji jamii juu ya matumizi bora ya vyandarua, kinga ya malaria kwa wajawazito, kuzijua dalili za homa ya malaria na kuwahi kupata huduma katika vituo vya afya, sambamba na namna ya kuwakinga wajawazito kwa dawa za SP.
Aidha, vipaumbele vingine katika mradi huo ni kuboresha huduma za upimaji na utoaji wa huduma sahihi za tiba dhidi ya malaria kwa kufuata miongozo ya kitaifa na kuhakikisha upatikanaji wa dawa mseto (ACTS) pamoja na vitendanishi na hadubini.

Jumatatu, Machi 27, 2017

MALARIA INAVYOZIDI KUTEKETEZA WATU NCHINI ZIMBABWE

Wizara ya Afya ya Zimbabwe imetangaza kuwa watu wasiopungua 150 wamefariki dunia kwa ugonjwa wa malaria nchini Zimbabwe katika muda wa miezi miwili iliyopita.
Wizara ya Afya ya Zimbabwe ilisisitiza jana Jumatatu kuwa, watu karibu elfu 90 wamegunduliwa kuwa na malaria huko Zimbabwe katika muda wa miezi miwili iliyopita.
Wizara hiyo imeongeza kuwa mvua kubwa zilizonyesha nchini Zimbabwe hivi karibuni ni sababu ya kushuhudiwa ongezeko la ghafla la malaria ambapo idadi kubwa ya watu wameugua ugonjwa huo.
Wizara ya Afya ya Zimbabwe imetaja sababu zilizopelekea kuongezeka wahanga wa maradhi hayo kuwa inatokana na kushindwa kufika wagonjwa katika vituo vya afya kwa ajili ya matibabu.
Takwimu za hivi karibuni zilizotolewa na maafisa wa Zimbabwe zinaonyesha kuwa, mvua kubwa zilizonyesha nchini humo zimeuwa watu wasiopungua 46 na kuwafanya wengine 2000 kukosa makazi. Serikali ya Zimbabwe imeomba msaada kwa jamii ya kimataifa ili kukabiliana na mfumuko wa ugonjwa huo. 

Jumapili, Machi 26, 2017

MWANAMITINDO ALIYEUGUA 'UGONJWA WA PAKA'

Mwanamitindo Caitin Stickels ana tatizo nadra sana la kiafya ambalo hufahamika kama 'Ugonjwa wa macho ya paka' ambalo humsababishia maumivu makali sana.
Lakini bado hajakata tamaa.
Tatizo hilo la kiafya humfanya aonekane kama paka.
Hali yake ilimvutia mpiga picha za mitindo kutoka Uingereza Nick Knight.
Alimtazama mwanamitindo huyo wa miaka 29 kutoka Seattle mara ya kwanza kwenye Instagram.
Tangu wakati huo, amevuma kama mwanamitindo na hata picha zake zikachapishwa katika jarida la V Magazine.
"Ni mabadiliko makubwa zaidi mema yaliyowahi kutokea katika maisha yangu," aliambia BBC.
Ugonjwa huo wa macho ya paka hufahamika kitaalamu kama Schmid-Fraccaro Syndrome.
Watu wenye ugonjwa huo wanaweza kuwa na matatizo katika maumbile ya masikio yao, moyo na kwenye figo.
Wakati mwingine, viungo vingine mwilini huathiriwa.
Sura ya Caitin si kama ya wanamitindo wengi ambao wamevuma sana.
'Urembo' wake si kama ule wengi waliozoea kuona ukiangaziwa kwenye majarida, filamu na runinga.
"Sikuwahi kuwa na ndoto ya kuwa mwanamitindo au kufikiria ningeshiriki katika tasnia ya mitindo na mavazi,"
"Mahangaiko mengi kwangu kutokana na ugonjwa huu huwa ni ndani ya moyo wangu," anasema.
"Nafikiri jambo jingine ni kwamba macho yangu huwa hawayumbuki kivyake; na hivyo hukaa kama ya paka wakati wote.
"Hii hata hivyo huniwezesha kuona vyema usiku, ninaweza nikatatizwa na jua kali. Nalipenda jua na mara nyingi hutokea nje na kutembea, lakini hilo hutatiza macho yangu."
Caitin anasema pia hupata maumivu makali mwilini na kupata kichefuchefu.
"Mwili wangu huathiriwa sana na mabadiliko katika mazingira, lakini kwa sababu umekuwa hivyo kwa muda mrefu, watu wengi niliotangamana nao huwa hawatambui kwamba kuna tatizo. Mimi ni mgumu kama jiwe."
"Kazi yangu ya uanamitindo, uigizaji na uimbaji hunisaidia sana kusahau maumivu niliyo nayo moyoni.
"Ni figo moja pekee yangu inayofanya kazi, kwa hivyo huwa inanibidi kunywa maji sana.
"Na sura yangu? Watoto wakati mwingine ndio hunishangaa. Lakini sana huwa sikabiliwi na unyanyapaa.
"Utoto wangu ulikuwa vile vile. Watoto ni watoto tu, ni kweli walinicheka na kunichezea. Lakini nani hakufanyiwa hivyo?"
"Sote huwa na kasoro pahala fulani na sote ni watu binafsi. Hakuna aliyekamilika," anaongeza.
"Jambo moja ni kwamba sote hatufanani na hakuna asiye na doa pahali."

BBC

Jumatano, Machi 22, 2017

KIPINDUPINDU CHAZUKA ZAMBIA

Ugojwa wa Kipindupindu umezuka katika wilaya mbili za Kaskazini mwa Zambia, huku watu 70 wakilazwa hospitalini, Wizara ya Afya ya nchini imetoa tarifa Jumanne.
Wezi Kaonga, Kaimu msemaji wa Wizara ya Afya, alisema kipindupindu kilizuka katika wilaya za Chiengi na Mpulungu ingawa hakuna vifo zimerekodiwa hadi sasa.

Jumatatu, Machi 20, 2017

MADAKTARI WA TANZANIA WAMEGOMA KWENDA KUFANYA KAZI KENYA

Chama cha Madaktari nchini Tanzania kimepinga mpango wa kuwatuma madaktari 500 nchini Kenya wakisema Tanzania ina upungufu mkubwa wa madaktari.
Hii inafuatia makubaliano kati ya serikali ya Tanzania na Kenya mwishoni mwa wiki ambapo madaktari wapatao 500 watapata ajira nchini Kenya.
Kenya imeshuhudia mgomo wa madaktari uliomalizika wiki jana baada ya mgomo huo kudumu kwa siku 100.
Miongoni mwa mengine, maafisa wa MAT wamesema wanahitaji ufafanuzi kuhusu ni kwa nini Serikali ya Kenya imeshindwa kuajiri Madaktari wake na kuanza kutafuta Madaktari kutoka Tanzania huku ikizingatiwa kwamba malipo ya Madaktari wa Tanzania yatakuwa makubwa zaidi ya wenyeji.
Aidha, mbona ombi hili limefanyika kipindi cha mgomo, na utekelezaji wake umekuja siku chache baada ya kuweka makubaliano ya kusitisha mgomo.
"Kwa nini suala hili linafanyika wakati wa kuelekea katika Uchaguzi Mkuu 2017? Ni nani atawajibika katika suala la usalama wa raia wetu, ikizingatiwa kwamba tayari kuna viashiria vya chuki, na ikizingatia Kenya bado ina changamoto za kiusalama," taarifa kutoka kwa chama hicho ilisema.
Chama hicho pia kinataka kujua ni kwa jinsi gani Madaktari wataweza kufanya kazi bila kukamilisha taratibu za kisheria kama vile kufanya mitihani ya Bodi na kusajiliwa ilikupata uhalali wa kutibu.
"MAT inasisitiza kwamba ni muhimu kusitisha zoezi la kuwapeleka Madaktari wa Tanzania mpaka hapo Serikali ya Kenya itakapoanza utekelezaji wa makubaliano kati yake na Madaktari wao," chama hicho kimesema.
"Serikali ya Tanzania itafute namna ya kuwaajiri madaktari wake ili kuziba pengo kubwa la upungufu wa madaktari nchini (Tanzania)."
Serikali ya Kenya imetetea hatua yake ya kutoa nafasi za ajira kwa madakatari kutoka nji za nje kuboresha sekta ya afya. Hii ni baada ya muungano wa madaktari KMPDU, kuishtumu serikali kwa kufanya uamuzi huo na kuwapuuza matatabibu wake wasio na ajira.
Waziri wa afya Cleopha Mailu aliyezungumza baada ya kuzuru hospitali kuu ya taifa ya Kenyatta mjini Nairobi Jumatatu, alipinga madai hayo na kusema kuwa matabibu wa Kenya huajiriwa wanapomaliza masomo na kuwa madakatari wasioajiriwa ni kwa hiari yao.
"Si ukweli kuwa tumewapuuza madaktari wetu wasio na ajira. Madaktari wa Kenya wakitoka shule, wanaajiriwa, yule ambaye yuko barabarani na hana ajira, ni jukumu lake, au ni hiari yake yeye mwenyewe. Au alitoka kwa serikali akaenda hospitali za kibinafsi".
Aidha, Waziri huyo, amewahakikishia madaktari kutoka nchini jirani kama vile Tanzania, kuwa hawatahitajika kupitia taratibu kama vile kutahiniwa. Hii ni baada ya uvumi kuenea kuwa madaktari hao wangelazimika kufanya mtihani kama inavyohitajika.
"Daktari wa Tanzania, Uganda, Rwanda na Burundi wanaweza kufanya kazi mahali popote bila kufanya mtihani na bila kudhulumiwa; kwa sababu shule zote zinakaguliwa pamoja, na wana mtala sawa," alisema.
Kenya imeahidi kuwa itaendelea kuwasaka madaktari zaidi kutoka mataifa ya afrika na mataifa mengine ili kufanuikisha huduma bora. Sekta ya afya nchini humo iliathirika zaidi baada ya madaktari kugoma kwa siku mia moja na kulemaza utoaji wa huduma za afya nchini humo.
Hata hivyo, shughuli za kawaida zimerejea katika hospiali hizo.

Jumapili, Machi 19, 2017

WAKENYA WAKATAA MADAKTARI KUTOKA TANZANIA

Muungano wa Madaktari Kenya (The Kenya Medical Practitioners and Dentists Union - KMPDU) umepinga hatua ya serikali kuajiri madaktari toka Tanzania.
Wanasema kama Serikali ya Kenya wanahitaji Madaktari, wawaajiri kwanza madaktari 1,400 waliomo Nchini Kenya.
Tanzania imetoa Madaktari 500 kuitikia ombi la rais wa Kenya Uhuru Kenyata.
Hivi karibuni Kenya ilikumbwa na Mgomo mkubwa wa Madaktari wakishinikiza nyongeza ya Mshahara.

KMPDU Secretary General Ouma Oluga Criticises Government for Bringing Doctors From Tanzania
By JULIET MUTAHI
Kenya Medical Practitioners, Pharmacists and Dentists Union (KMPDU) Secretary General Ouma Oluga, has issued a new demand after Tanzanian President John Magufuli offered to send 500 doctors to Kenya.
Oluga demanded that the foreign medics must go through several procedures including undergoing an examination before they start working in the country.
The Secretary General criticised the government for seeking outside help yet there were many unemployed medical practitioners in Kenya.
He wondered why the government had to source for doctors from Tanzania yet it would pay the same money the local medics had been demanding for.
"Kenya has about 1,400 doctors awaiting employment. It would be very costly and therefore a show of imprudent public finance management to have 500 Tanzania doctors at Sh20,000 per day," 
he said. At the same time, Dr Oluga accused the government of failure to retain doctor's in hospitals due to lack of proper working conditions.
He, however, assured that KMPDU would welcome the foreign practitioners and register them into the Union.
Earlier in the day, Magufuli had agreed to offer the 500 medics to help mitigate the effects of the recently called off strike following a request by President Uhuru Kenyatta.
He stated that there were many qualified and unemployed doctors who were ready to offer their services in Kenya.
Source: Government Issued New Demand After Magufuli Gives Kenya 500 Doctors

Jumamosi, Machi 18, 2017

TANZANIA KUPELEKA MADAKTARI 500 KENYA

Serikali ya Tanzania imekubali ombi la Kenya la kuisaidia nchi hiyo na madaktari 500 watakaosaidia kukabiliana na tatizo la uhaba wa madaktari katika vituo vyake vya tiba kufuatia kutokea kwa mgomo wa madaktari nchini humo.
Rais wa taifa hilo John Pombe Magufuli amekubali kutoa madaktari hao baada ya kufanya mazungumzo na ujumbe wa Kenya wa maafisa wa afya uliotumwa kwake na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Kiongozi huyo amesema kuwa Tanzania imekubali ombi hilo kwa kuwa Kenya ni jirani ,ndugu na rafiki wa kweli wa Tanzania na amemtaka waziri wa afya nchini humo Ummy Mwalimu kuharakisha mchakato huo ili maafisa hao waelekee Kenya kutekeleza jukumu hilo.
Serikali ya Tanzania imekubali ombi la Kenya la kuisaidia nchi hiyo na madaktari 500 watakaosaidia kukabiliana na tatizo la uhaba wa madaktari katika vituo vyake vya tiba kufuatia kutokea kwa mgomo wa madaktari nchini humo.
Rais wa taifa hilo John Pombe Magufuli amekubali kutoa madaktari hao baada ya kufanya mazungumzo na ujumbe wa Kenya wa maafisa wa afya uliotumwa kwake na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Kiongozi huyo amesema kuwa Tanzania imekubali ombi hilo kwa kuwa Kenya ni jirani ,ndugu na rafiki wa kweli wa Tanzania na amemtaka waziri wa afya nchini humo Ummy Mwalimu kuharakisha mchakato huo ili maafisa hao waelekee Kenya kutekeleza jukumu hilo.
''Matatizo ya Kenya ni matatizo ya Tanzania, tutawapatia madaktari hao 500 wakatoe huduma kwa ndugu zetu waliopo Kenya na kwa kuwa mumenihakikishia kuwa madaktari wangu watalipwa mishahara inavyostahili, kufanya kazi katika mazingira mazuri mbali na kuwapa nyumba za kuishi, sina tatizo naamini mambo yatakuwa mazuri'', alisema Magufuli.
Waziri wa afya wa Kenya Dkt. Cleopa Mailu ambaye aliongoza ujumbe huo alimweleza rais Magufuli kwamba baada ya mgomo wa madaktari pamoja na uamuzi wa taifa hilo kugatua madaraka katika sekta ya afya imebainika kuwa taifa hilo lina uhaba mkubwa wa madaktari ambao hauwezi kumalizwa kwa kutegemea madaktari wanaosomeshwa nchini humo bali kupata madaktari kutoka nje.
Mheshimiwa Jack Ranguma ambaye alikuwa katika ujumbe huo wa Kenya amesema kuwa Kenya itawalipa madaktari hao kwa stahili zote ikiwa ni mishahara na nyumba za kuishi.
Naye waziri wa afya na ustawi wa jamii nchini Tanzania Ummy Mwalimu amesema kuwa wizara yake iko tayari kutoa madaktari hao haraka iwezekananvyo akisema kuwa Tanzania ina madaktari wengi wazuri ambao wamehitimu lakini hawajapata ajira, huku wengine wakimaliza mikataba yao ya kazi wakiwa na uwezo wa kufanya kazi.
''Kwa hiyo nitoe wito kwa madaktari wote nchini Tanzania ambao hawapo katika utumishi wa umma, hawapo katika hospitali teule na ambao hawapo katika hospitali za mashirika yasiokuwa ya serikali wanaolipwa na serikali waombe nafasi hizi''
''Vigezo tunavyaongalia ni kwanza awe amemaliza mafunzo ya vitendo yani Internship, pili awe amesajiliwa na baraza la madaktari la Tanganyika. Kwa hiyo leo hii tunatoa tangazo na tumefurahi sana kwa sababu tuna madaktari wa kutosha ndani ya nchi na tunaweza kuwapeleka Kenya'',alisema muheshimiwa Ummy.

Jumamosi, Machi 11, 2017

MADAKTARI WA TANZANIA WAGOMA KUAJILIWA KENYA

Madaktari nchini Tanzania hapo jana ( Ijumaa) walikataa mpango na serikali ya Kenya kuwaajiri hili kujaza pengo iliyoundwa na madaktari amabo wako kwa mgomo nchini umo.
Elisha Osati, Mwenyekiti mteule wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), alisema kinyume na hatua hiyo, akisisitiza kwamba walikuwa tayari tu kwa hiyo hatua baada ya mgomo kumalizika na si sasa.

Jumatano, Machi 01, 2017

USHOGA MFUPA MGUMU KWA KIGWANGALLA?

Tanzania imerudi nyuma katika uamuzi wake wa hapo awali wa kutangaza hadharani majina ya mashoga wanaouza huduma za ngono kwenye mitandao ikisema kuwa hatua hiyo huenda ikaharibu ushahidi dhidi ya washukiwa hao.
Naibu waziri wa afya Hamisi Kigwangalla alisema kuwa serikali itashughulikia swala hilo na kutoa taarifa kwa umma baadaye. 
Awali Kigwangalla aliratibiwa kutoa orodha ya mashoga wanaouza huduma za ngono mitandaoni katika mkutano wake na waandishi wa habari siku ya Jumatatu. 
Kigwangalla alisema kutangaza majina ya washukiwa hao ni kama “kufungulia shetani ambaye tayari amewekwa ndani ya chupa”.

Jumatatu, Februari 27, 2017

HOMA YA MAFUA YA NGURUWE YAPATIKANA TANZANIA

Mlipuko wa ugonjwa wa homa ya mafua ya nguruwe umeikumba wilaya ya Kalambo mkoa wa Rukwa kusini magharibi mwa Tanzania, na kusababisha vifo vya nguruwe karibu 200.
Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Bibi Julieth Binyura amesema serikali imepiga marufuku biashara ya nyama hiyo, na usafirishaji wa nguruwe hai ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa huo. Bibi Binyura pia amesema wanavijiji wa wilaya hiyo wamearifiwa kuhusu ugonjwa huo. Ofisa mifugo wa Wilaya hiyo Bw Wilbrod Kansapa amesema nguruwe wanaoonekana wakirandaranda wanakamatwa.
Ufugaji wa nguruwe unaendelea kuongezeka katika maeneo ya magharibi mwa Tanzania, kutokana na mahitaji makubwa kwenye miji mikubwa kama Dar es salaam.

Jumapili, Februari 12, 2017

MWANAMKE MNENE ZAIDI DUNIANI KUPASULIWA ILI KUPUNGUZWA UZITO

Mwanamke mzito zaidi duniani, akiwa na uzani wa kilo 500, amefikishwa nchini India atakapofanyiwa upasuaji wa kumsaidia kupunguza uzani.
Eman Ahmed Abd El Aty, mwenye umri wa miaka 36 alifika mjini Mumbai jana (Jumamosi) kutoka mji wa Alexandria nchini Misri. 
Ripoti kutoka kwa jamaa zake zimedokeza kwamba Abd El Aty hajatoka nyumbani mwake kwa zaidi ya miaka 25 kwa sababu ya kushindwa kudhibiti uzani wake. 
Abd El Aty alinyimwa visa na ubalozi wa India mwaka uliopita kwa sababu hangeweza kufika katika ubalozi huo. 
Hatimaye alipata visa baada ya daktari wake kuzungumzia hali yake kwa waziri wa mambo ya nje.