Alhamisi, Mei 08, 2014

NYOTA YAKO LEO ALKHAMISI TAREHE 8/05/2014:

NG’OMBE – TAURUS (APR21 – MAY 20)
Siku ya leo kuna kila dalili kuwa maisha yako yatakuwa mazuri, maradhi au matatizo madogomadogo yatapungua. Vilevile Mkeo au mumeo atakufurahisha kwa zawadi atakayokupa alkhamisi ya leo.

MAPACHA - GEMINI (MAY 21- JUN 21)
Mchana wa leo utapokea habari za kutatanisha kuhusu kazi yako mambo yako ambayo yalikuwa yanakutatiza usiyaguise yanaweza kuleta matata., unashauriwa usianzishe biashara ya aina yeyote kwa wakati huu.

KAA - CANCER (JUN 22- JUL 22)
Usipokuwa makini alkhamisi ya leo kuna dalili ya kuwa mambo yako yatafuatiliwa na watu bila ya wewe mwenyewe kujua, kuwa mwangalifu kwa kila hatua utakayoichukua. Kuna mtu unayemuamini sana unatakiwa uwe muangalifu naye anaweza akakudhuru.

SIMBA - LEO (JUL 23 –AUG 22)
Leo kuna kila ishara ya kukwama kwa mipango yako ya kipesa, mipango ya ndoa au mapenzi itaendelea kama kawaida na kuna mwanamme mrefu mweusi ukikutana naye hiyo itakuwa ni dalili ya kufanikiwa kwa kila jambo.

MASHUKE - VIRGO (AUG 23- SEPT 23)
Leo kuna dalili kuwa mambo yako hayatakuwa safi na utachukiwa na na kila mtu hapo kazini kwako au mtaani kwenu. Jitahidi kuandaa tafrija na uwakirimu watu ili upate baraka na mikosi ikuondoke.

MIZANI - LIBRA (SEPT 24- OCT 23)
Leo kuna kuingiliwa katika kazi zako au kusimamishwa kufanya yale uliyokuwa umeyapanga kuyafanya. Vilevile kuna dalili ya kukimbiwa na Mpenzi wako, unashauriwa kuwa mpole na mwenye subira ili ufanikiwe.

NGE - SCORPIO (OCT 24- NOV 22)
Leo naona unafikiria mambo ya kushirikiana au kazi na kipato. Ipo dalili kuwa mambo yako kufunguka na mikosi kuonoka. Unashauriwa usijaribu kuingia katika biashara inayoendeshwa na ndugu yako

MSHALE - SAGITARIUS ( NOV 23 - DES 21)
Mchana wa leo naona una taabu na magomvi, unalaumiwa na ugonjwa unakutatiza kuna ishara ya kupata mali itakayotokana na urithi au kukabidhiwa mali ya watu uitunze. Lazima katika mambo yako uwashirikishe ndugu zako ndio utafanikiwa.

MBUZI - CAPRICORN (DES 22 – JAN 20)
Leo kuna dalili yakupata mali au kupewa pesa na watu uliokuwa umewafanyia kazi siku za nyuma lakini walikataa kukulipa. Kuna mpango wa safari uliokuwa unausubiri, mpango huo utafunguka baada ya siku tatu kuanzia leo.

NDOO –AQUARIUS (JAN 21 – FEBR 19)
Wiki hii mtoto wako ataugua na kuvuruga mipango yako na utavunjiwa heshima na rafiki yako ambaye hana heshima au wewe utapata maradhi ya kuumwa na kichwa. Kuepusha hayo safiri mbali kwa muda wa wiki.

SAMAKI – PISCES (FEB 20- MACH 20)
Kwanza ujue kuwa safari ukiwa nayo ni mbaya na mgonjwa yupo ndani ya shida kubwa.Mchana wa leo, hiyo ni dalili ya kwamba hutopata maradhi au kuugua kwa muda mrefu, vile vile ni dalili ya kuletewa zawadi kutoka kwa rafiki yako aliye mbali.

PUNDA- ARIES (MACH 21- APR 20)
Mchana wa leo hiyo ni dalili kwamba mambo yako mengi yatafanikiwa kwa kuwatumia watu wengine bila ya wewe mwenyewe kushiriki. Tegemea kukutana na mtu mkubwa Serikalini ambaye atakusaidia.

0 comments:

Chapisha Maoni