Alhamisi, Mei 08, 2014

MCHUNGAJI AMBAKA MTOTO WA MIAKA 13 JIKONI

Pepo la Wachungaji kutafuna Kondoo wao katika makanisa yao, limeibuka Upya, baada ya kuzima kwa Muda Kadhaa. Mchungaji TYRONE BANKS mwenye Umri wa Miaka 58, amewekwa Chini ya Ulinzi na kutupwa nyuma ya Nondo, baada ya
Kupatikana na hatia ya Kumbaka Binti wa Miaka 13 (Jina tumelihifadhi), ambaye anatokea katika familia Rafiki.
Ripoti imezidi kumiminika kuwa, Pastor Huyo kutoka Huko ALABAMA, alikuwa ameshajijengea Uaminifu kwa Binti huyo, lakini alikuja kuharibu baada ya kutekeleza kitendo hicho kibaya kilichosababisha madhara kwa binti huyo.
Aidha Story kamili ni Kwamba, Pastor Tayrone, alimchukua Binti huyo katika gari lake, na kuenda naye katika kanisa Linalofahamika kwa jina la HUEYTOWN. Baada ya kufika huko, Mchungaji huyo alimshawishi Binti huyo waingie Ndani, na Baada ya Kuingia tu, Alifunga Mlango kwa Funguo, na Kutekeleza tukio hilo Kinyume na Kazi yake, Heshima yake, Hadhi yake, pamoja na Sheria.
Baada tu ya Binti huyo kurudishwa Nyumbani, Moja kwa Moja alimuambia mama ake kilichotokea, huku akithibitisha kuwa alifanyiwa kitendo hicho cha Kinyama Katika Maeneo ya jikoni , ndani ya kanisa hilo.
Mpaka hivi sasa, Mchungaji Tyrone amefunguliwa mashitaka ya UBAKAJI, na yuko Mikononi mwa Polisi.

0 comments:

Chapisha Maoni