Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesikitishwa sana na ujumbe wenye
maudhui ya ubaguzi ulioandikwa kwenye moja ya Bango lililobebwa na mmoja
wa wananchi waliojitokeza katika maadhimisho ya Sherehe za Miaka 52 ya
Mapinduzi ya Zanzibar.
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinaomba radhi
kwa ujumbe huo, kinapinga na kinakemea kabisa fikra, hisia na mitazamo
yoyote yenye maudhui ya kibaguzi.
Ujumbe huo sio tu kuwa una maudhui ya kibaguzi bali pia unaenda kinyume
kabisa na falsafa na Shabaha ya waasisi wa Mapinduzi hayo Matukufu ya
mwaka 1964 na unapingana na misingi na itikadi ya CCM inayohimiza Umoja
na Mshikamano wa Kitaifa.
0 comments:
Chapisha Maoni