UMOJA
wa vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), umekitaka chama hicho kumvua
uanachama Rais mstaafu wa Zanzibar Dk Amani Abeid Karume.
Kauli hiyo imetolewa katika viwanja vya Maisara mjini Zanzibar na
Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Sadifa Juma Khamis wakati wa kilele cha
matembezi ya vijana wa umoja huo kuadhimisha miaka 52 ya Mapinduzi.
Alimshushia tuhuma nzito mstaafu huyo kuwa anashirikiana na wapinzani
kukihujumu chama hicho kikongwe nchini, na kwamba asipofukuzwa umoja
umoja huo utatumia njia zingine ambazo hakuziweka wazi.
Sadifa alionya kwamba Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar si mali wala miliki
ya mtu kwani Wazanzibar wote wana haki ya kushiriki kuyaenzi kwa
vitendo kutokana na historia yake.
0 comments:
Chapisha Maoni