Jumanne, Januari 12, 2016

KUHUSU MAONESHO YA MAGARI YA KIFAHARI


Wapenzi wa gari za kisasa waliohudhuria maonyesho ya kimataifa ya magari jijini Detroit, Marekani walivutiwa na ubunifu wa teknolojia za kisasa kwenye magari yaliyokuwa katika maonyesho hayo, ikiwemo magari yaliyo na uwezo wa kujiendesha bila dereva.
Magari ya Ford na Volvo yaliongoza katika ubunifu wa teknolojia huku kampuni hizo mbili zikionyesha teknolojia ya juu zaidi ya kuzuia visa vya ajali na magari yanayojiendesha.
Jeshi la Marekani pia lilileta lorry yake yenye uwezo wa kujiendesha, lakini teknolojia hio bado haitatolewa kwa matumizi ya umma.

0 comments:

Chapisha Maoni