Jumanne, Septemba 17, 2013

MIRADI YA NYUKLIA YA IRAN, MKAKATI WA MAENDELEO ENDELEVU

Mwakilishi wa Iran katika Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) amesema katika kikao cha Bodi ya Magavana ya wakala huo kwamba, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko tayari kuimarisha uhusiano wa karibu na taasisi hiyo ili kutatua kila aina ya utata uliopo kuhusu miradi yake ya nyuklia. Redha Najafi pia amesema, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitofumbia macho haki yake ya kustafidi na nishati ya atomiki kwa matumizi ya amani.
Mwishoni mwa kikao hicho cha msimu cha Bodi ya Magavana, sambamba na kusisitizia majukumu na matarajio ya nchi wanachama wa Mkataba wa N.P.T mkabala wa IAEA, mwakishi huyo wa Iran amebainisha malengo yanayofuatiliwa na Iran katika kutumia nishati ya atomiki.
Lengo la kwanza la Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (IAEO) ni kuzalisha umeme yaani kuwa na nishati salama inayotokana na nguvu za nyuklia.
Katika kufanikisha hilo kiwanda cha kwanza cha atomiki cha Iran cha Bushehr kilichopo kusini mwa nchi, chenye uwezo wa kuzalisha Megawati 1000 za umeme wiki ijayo Septemba 24 kitakuwa tayari kwa ajili ya kukabidhiwa kwa kandarasi wa Kiirani.
Ama lengo la pili la Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran ni kuzalisha fueli kwa ajili ya tanuri yake ya utafiti ya Tehran sambamba na kulinda mzunguko wa kuzalisha fueli ya nyuklia.
Hakuna shaka kuwa, kurutubisha urani hakukinzani na sheria za IAEA wala Mkataba wa NPT, na Iran inataraji kuwa haki yake hiyo itatambuliwa rasmi na wakala huo. Nchi za Magharibi na zenye kumiliki fueli ya nyukilia, huku zikiwa na malengo ya upendeleo yamelenga miradi ya nyuklia ya Iran, na tangu miaka miwili iliyopita yamekataa kuidhaminia fueli tanuri ya utafiti ya Tehran.
 Lakini huku baadhi wakiamini kuwa, uzalishaji fueli hiyo unahijia miaka isiyopungua miwili na nusu, wanasayansi wa Kiirani wameweza kufanikisha jambo hilo katika kipindi cha miezi 18.
Ili kufikia dhumuni hilo la kisayansi, Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran limetekeleza kwa mafanikio awamu ya mwanzo ya mradi mkubwa wa mzunguko wa fueli nyuklia ambao ni takwa la kitaifa, kwa kuanzisha kiwanda cha nyuklia cha Isfahan na mradi wa tanuri la maji mazito huko katika mkoa wa Arak.
Mwaka uliopita pia kulianzishwa kiwanda cha kurutubisha madini ya urani cha Fordu karibu na mji wa Qum, ambacho kiko chini ya usimamizi kamili wa IAEA. Hivi sasa fueli inayotumika katika tanuri ya utafiti ya Tehran imetengenezwa na wanasayansi wa Kiirani, suala ambalo limeondoa haja ya Iran kuzitegemea nchi zinazozalisha urani iliyorutubishwa kwa asilimia 20.
Katika ripoti mpya ya Yukia Amano Mkurugenzi Mkuu wa IAEA katika kikao cha Bodi ya Magavana ilitangazwa kawa, mashinepewa za kizazi kipya zilizozalishwa ndani ya Iran zinafanya kazi katika viwanda vya nyuklia hapa nchini.
Hivi sasa aina 15 za dawa za tiba ya mionzi zinazalishwa nchini Iran na kutumika katika matibabu ya wananchi milioni moja wanaosumbuliwa na magonjwa ya saratani.  Hali kadhalika, ili kuzalisha fueli inayohitajika katika viwanda vyake zaidi ya 20, inakadiriwa kuwa Iran inahitaji tani 30 elfu za fueli ya nyuklia suala ambalo linathibitisha mkakati wa maendeleo ya Iran kwa ajili ya kuzalisha Megawati zisizopungua 20 elfu za umeme.
Marekani na washirika wake kwa kutumia vikwazo, mashinikzo ya kisiasa, vitisho vya kijeshi na hata kuwaua wanasayansi wa nyuklia wa Iran na pia kukwamisha miradi hiyo kwa kushambulia kwa virusi mitambo ya nyuklia, wanafanya njama za kuzuia mwenendo wa maendeleo na uvumbuzi katika teknolojia ya nyuklia inayotumiwa na Iran kwa malengo ya amani.
Lakini licha ya ukwamishaji huo wa nchi za Magharibi, teknolojia ya nyukilia hii leo ni moja ya mafanikio muhimu zaidi ya kisayansi yaliyopatikana katika taifa la Iran

0 comments:

Chapisha Maoni