Jumanne, Septemba 23, 2014

MABADILIKO MAKUBWA KATIKA BUNGE MAALUM LA KATIBA

Bunge Maalumu la Katiba la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha azimio la kuzifanyia marekebisho kanuni za 30, 36 na 38 ili kuruhusu wajumbe watakaokuwa nje ya Bunge iwe ndani au nje ya nchi, wapige kura za kuamua ibara na sura za rasimu ya katiba popote watakapokuwa. Kwa mabadiliko hayo, wajumbe wa Kiislamu waliokwenda kutekeleza ibada ya Hija Makka Saudi Arabia, wanaopata matibabu nchini India na walio katika majukumu mengine ndani na nje ya nchi, watapiga kura kuamua rasimu ya katiba mpya inayopendekezwa. Hata hivyo mabadiliko hayo yalizua mjadala na mvutano mkali kati ya Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samuel Sitta na baadhi ya wajumbe wa Bunge hilo maalumu la Katiba. Taarifa zaidi kutoka ndani ya Bunge la Katiba zinasema kuwa, Septemba 25 wajumbe watakaa kwenye kamati kuona kama mapendekezo yao yamewekwa ipasavyo kwenye rasimu hiyo na baada ya hapo Septemba 27 na 28, kamati ya uandishi itaiweka sawa rasimu hiyo ili Septemba 29 hadi Oktoba 2 mwaka huu, ipigiwe kura.

0 comments:

Chapisha Maoni