Baraza la Wazee wa Klabu ya Young Africans leo wamefanya mkutano na
waandishi wa habari makao makuu ya klabu na kuwakemea wanachama
wanaosema ya kwamba watapeleka baarua TFF kwa ajili ya kuushitaki
uongozi kuwa wamevunja Katiba kwa kuongeza muda wa mwaka mmoja kuwa
madarakani.
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu, Katibu wa
Baraza la Wazee Bw Ibrahim Akilimali amesema kwa niaba ya Baraza la
Wazee wanasema wanachama wanaopinga maamuzi ya mkutano mkuu uliokuwa na
wanachama zaidi ya 1500 basi wafuate taratibu za kuwasilisha malalamiko
yao ni si kufanya vinginevyo.
Mwenyekiti wetu Yusuf Manji alishasema tangu mapema ya kwamba yeye hatagombea tena na siku ya mkutano aliyasema hayo awali, lakini Mjumbe wa Baraza wa Wadhamini mzee Jabir Katundu aliwasilisha hoja ya kumuomba aendelee na uongozi, ndipo wanachama walipopata nafasi ya kujadili chini ya Mama Karume na kwa pamoja kuafiki Mwenyekiti aendelee japo kwa miaka minane
alisema
Akilamali.
Aidha Akilimali alisema Manji hakuafikiana na suala
hilo na ndipo alipoomba japo aongezewe muda wa mwaka mmoja kabla ya
kuelekea kwenye mikikimikiki ya Uchaguzi ili aweze kukamilisha baadhi ya
mambo kama ya usajili, ujio wa kocha mkuu mpya Marcio Maximo na ujenzi
wa Uwanja.
Naye mwenyekiti wa Baraza la Vijana Bw Bakili Makele
amesema wao kama vijana pia wanashangazwa hao baadhi ya wanachama ambao
wanataka kuirudisha Yanga nyuma, mara hii wameshasahau shuruba
tulizopitia mpaka kufikia muafaka, sisi kama vijana tunasema hatuamini
kama hao wanaosema hawakubaliani na maamuizi ya mkutano ni watu
wanaoitakia mema klabu yetu.
Mwenyekiti Bw Yusuf Manji hajayapenda madaraka na wala haitaji kuendelea kuiongoza Yanga, bali kwa maombi yetu sisi wanachama pamoja na Baraza la Wadhamini alikubali kuiongoza japo kwa mwaka mmoja kabla ya kuelekea kwenye mkutano mkuu wa Uchaguzi ambapo atakayejiona ana uwezo wa kuongoza Yanga basi atapata fursa hiyo ya kujinadi na si kupiga kelele sasa hivi kweye vyombo vya habari
alisema Bakili.
0 comments:
Chapisha Maoni