Shirika la kutoa huduma za kibinadamu Oxfam
limeendesha kile inachosema ni 'kombe la dunia mbadala' kuangazia pengo
linalozidi kuwa kubwa kati ya maskini na matajiri katika mataifa
yanayoshiriki kombe la dunia mwaka huu.
Ubelgiji imetangazwa mshindi kwa sababu si kuwa
ina utajiri si haba bali pia ina mwanya mdogo zaidi kati ya raia wake
matajiri na wenye kipato, ilhali wenyeji Brazil imefeli hata kufuzu
raundi ya pili kwa jinsi pengo la umaskini na matajiri lilivyokumbwa
miongoni mwa raia wake.
Mataifa mengineyo ya America kusini pia
hayajafanya vizuri lakini yanasemekana kujitahidi, cha ajabu mataifa ya
kiafrika yanayoshirki kombe la dunia hayajatajwa.
0 comments:
Chapisha Maoni