Alhamisi, Juni 12, 2014

UTABIRI MZITO ZAIDI WATOLEWA JUU YA VIFO VYA MASTAA, MWEZI HUU KUFA 20, NI KUTOKA KWA NABII...MAFUTA MATAKATIFU YATAJWA KUWA KINGA

Achana na Maalim Hassan, safari hii ameibuka Nabii wa  Huduma ya Ufufuo iliyopo Buza jijini Dar es Salaam, Yaspi Paul Bendera (pichani)  ambaye amekazia kuwa vifo kwa wasanii wa Kibongo vitaendelea.

Akizungumza bila Nabii Bendera alisema: 

Nimeona kwamba, ndani ya mwezi huu (Juni) watakufa wasanii 20. Huu si utani, ni maono.
Hakuna masharti magumu, Mungu anawapenda wasanii, lakini ikiwa wanataka kuepukana na vifo ninavyoviona mimi, waje kanisani kwangu niwapake mafuta matakatifu.
Wanatakiwa kumgeukia Mungu sasa, hali siyo nzuri. Nasisitiza waje niwapake mafuta matakatifu, vinginevyo wataendelea kupukutika.
Nabii huyo aliendelea: 
Kuna msanii mmoja anasali kanisani kwangu, anaitwa Herieth (Chumila). Nilimpa huu ujumbe awafikishie wenzake. Anayepuuza na apuuze lakini nawahakikishia wakimgeukia Mungu haya mabalaa hayatawakumba kamwe.
Baada ya hayo naye Herieth ‘Mama wa Bongo Muvi’ athibitisha kuwa kweli alipewa ujumbe huo na Nabii Bendera awafikishie wenzake.
Ni kweli nasali pale, ni kweli pia nilitumwa na Nabii Bendera nikazungumze na wasanii wenzangu kuhusiana na maono aliyooneshwa.
Naamini utabiri wake kwa sababu nasali pale na siku aliyotabiri mambo hayo ndiyo siku aliyofariki  dunia Mzee Small, nawashauri wasanii wafuate ushauri huo, waende tu kwani wakipakwa mafuta hayatawadhuru kwa lolote kwa sababu  amekuwa akitabiri mambo mengi na yametokea
alisema Mama wa Bongo Muvi.
Licha ya utabiri huo wa aina yake wa Nabii Bendera, mchungaji mmoja wa makanisa ya kiroho ambaye hakupenda jina lake liandikwe mtandaoni kwa kuhofia malumbano alipingana na utabiri huo akisema ni gia ya kutafutia waumini.
Hakuna kitu kama hicho. Aseme anataka kupata waumini wengi. Kama kweli yeye alioneshwa hayo maono kwa nini asiishie kuwaombea tu? Kwa nini amesema waende kanisani kwake akawapake mafuta na asiwaelekeze waende kwenye makanisa yaliyo karibu nao?
Huyo anataka waumini, asidanganye watu. Mungu ninayemwamini anaishi ndani ya nafsi ya mtu. Kama kweli aliona hayo, dawa yake yalikuwa maombi tu, siyo kwenda kupakwa mafuta, tena na yeye mwenyewe
alisema mchungaji huyo.

0 comments:

Chapisha Maoni