Jumatatu, Juni 02, 2014

TETESI ZA USAJILI KATIKA MAGAZETI YA LEO UINGEREZA

Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger anafikiria kumsaini striker wa AC Milan Mario Balotelli baada ya mchezaji huyo kuambiwa hahitajiki tena San Siro (Daily Mirror), Liverpool, Chelsea na Tottenham pia zinaweza kumfuatilia Balotelli (Daily Express), Arsenal wametupilia mbali nafasi ya kumsajili tena Cesc Fabregas, licha ya kuwa Barcelona wapo tayari kumuuza kwa pauni milioni 30 (Daily Mail), Manchester City ndio klabu inayoonekana inataka kumchukua Fabregas, huku Liverpool nayo ikimfuatilia, lakini Man United wako kimya ingawa walimtaka sana msimu uliopita (Daily Mirror), Juhudi za Liverpool kumsajili Adam Lallana zinasuasua baada ya Southampton kugoma kushusha bei ya pauni milioni 30 (Times), mazungumzo ya mkataba kati ya Chelsea na Frank Lampard yamegonga mwamba (Daili Express), Manchester City huenda wakampa Lampard mkataba mfupi kabla ya kuhamia Marekani katika klabu inayomilikiwa na City (Daily Mirror), Inter Milan inamtaka striker wa Man U, Javier Hernandez "Chicharito" kwa mkopo. 
Inter pia inamtaka Fernando Torres (Daily Mail), Swansea wamekubali kulipa pauni milioni 6.5 kumsajili mshambuliaji wa FC Twente, Luc Castaignos (Sky Sports), Liverpool wanakaribia kukamilisha usajili wa beki wa kushoto kutoka Spain Alberto Moreno (Daily Mirror), nahodha wa Swansea Ashely Williams yuko tayari kuhamia QPR (Daily Mail), Liverpool, Tottenham na Manchester United wanamfuatilia beki wa Feyenoord Stefan de Vrij (Daily Star), striker wa Spain David Villa ameondoka Atlètico Madrid na kuelekea New York, Marekani (Sun), kiungo wa Ufaransa Franck Ribery huenda akakosa kucheza Kombe la Dunia kutokana na majeraha ya mgongo (Metro) na Manchester City hatimaye wanatarajia kukamilisha usajili wa kiungo Fernando kutoka Porto kwa pauni milioni 12.2.

0 comments:

Chapisha Maoni