MWANAFUNZI wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Nyakabale
wilayani hapa (jina limehifadhiwa), ameamrishwa kula kinyesi chake
baada ya kukutwa akijisaidia kwenye kisima cha maji.
Kamanda wa Polisi mkoani Geita, Joseph Konyo, alisema jana kuwa mtu
mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Marco Maiko, alimwamuru mwanafunzi
huyo anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka nane, kula kinyesi hicho
alichokuwa amejisaidia karibu na kisima chake.
Kamanda Konyo alisema mwanafunzi huyo akiwa na wenzake watatu,
alijisaidia karibu na kisima hicho, na Maiko alimwamuru mwanafunzi huyo
akile hadi kiishe na kwa hofu ya kupigwa alitii na kukila kinyesi
hicho huku wenzake wakishuhudia.
Kamanda Konyo alisema baada ya kufika nyumbani, mwanafunzi huyo
alimwambia mama yake, Agnes Lujaja (26), juu ya kilichotokea, ndipo
mtuhumiwa alipokamatwa.
Alisema uchunguzi unaendelea, na kwamba mtuhumiwa atafikishwa
mahakamani kwa mashitaka ya kudhuru mwili. Mwanafunzi huyo alipelekwa
katika zahanati ya Nyakabale kwa matibabu zaidi.
0 comments:
Chapisha Maoni