Jumamosi, Juni 14, 2014

MCHUNGAJI MTIKILA ASHINDA KESI DHIDI YA SERIKALI, MAHAKAMA YAAMURU SERIKALI KUMTAMBUA MGOMBEA BINAFSI

MAHAKAMA ya Afrika inayoshughulikia masuala ya haki za binadamu, jana imetoa hukumu katika kesi iliyofunguliwa na Mchungaji Christopher Mtikila, ambayo italazimisha kusitishwa kwa Bunge la Katiba ili kupisha utekelezaji wa sehemu ya hukumu hiyo ambayo ni ya kikatiba.
Katika hukumu hiyo, mahakama imeitaka serikali kutekeleza kwa vitendo hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu Juni 14, mwaka jana katika kesi ya kudai mgombea binafsi katika uchaguzi wa ngazi zote, iliyofunguliwa na Mchungaji Mtikila dhidi ya serikali.
Akisoma hukumu hiyo, Rais wa majaji wa mahakama hiyo, Jaji  Sophia Akuffor, mbele ya wawakilishi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, alitaka serikali ndani ya miezi sita kwanza kutangaza katika gazeti la serikali hukumu iliyompa ushindi Mchungaji Mtikila ya mgombea binafsi na pia kutangaza hukumu hiyo katika wavuti ya serikali.
Jaji huyo aliitaka serikali kuwasilisha katika mahakama hiyo utekelezaji wa hukumu hiyo na kubainisha kuwa imeweka katika mchakato suala la mgombea binafsi ili kutekeleza hukumu hiyo.
Alisema pia katika matangazo hayo, hukumu hiyo iwe imetafsiriwa katika lugha nyepesi ya Kiswahili na Kiingereza ili kuwawezesha wananchi wote kuisoma vizuri.

0 comments:

Chapisha Maoni