Jumatatu, Juni 09, 2014

KUHUSUANA NA PICHA ZISIZO NA MAADILI MITANDAONI ZIKIWEMO ZA DIAMOND NA WEMA, HII NDIO KAULI TOKA BUNGENI DODOMA

Sakata la kusambaa picha zisizokuwa na maadili mitandaoni zikiwemo za watu maarufu hapa nchini leo limezungumziwa tena katika bunge la Tanzania kule Dodoma ambapo katika kipindi cha maswali na majibu Mhe. Habib Mnyaa ameonekana akihoji serikali inachukua hatua gani juu ya watu wanaotuma picha zao zisizo na maadili mitandani zikiwemo za kina Wema na Diamond wanazopiga wakiwa chumbani na kuweka kwenye mitandao.
Katika majibu yake waziri wa mawasiliano, sayansi na teknolojia Prof. Makame Mbarawa anasema 
Mhe. Spika kuhusu picha zisizokuwa na maadili zinazowekwa katika mitandao na watu maarufu na hata wasiokuwa maarufu serikali imeanza kuandaa kanuni zitakazokuwa zikifuatilia Online Content ambapo itaanza kuchukua hatua baada ya kufuatilia juu ya picha hizo na kuchukua hatua madhubuti.

0 comments:

Chapisha Maoni