Jumatatu, Juni 09, 2014

MAABARA ZA ARUSHA CHALI

Maabara ya shule ya sekondari ya arusha iliyowai kutoa viongozi wengi wa serikali na kituo cha sayansi kwa shule za sekondari za mkoa wa arusha ipo katika hali mbaya ya uchakavu unaosababisha maji ya mvua kuingia ndani hali inayodaiwa kuchangia kupunguza  ari ya  wanafunzi kujiunga na  masomo  ya sayansi.
Wakizungunza na wanahabari wanafunzi wa shule ya sekondari ya arusha wamesema uchakavu wa maabara hiyo umechangia kufifisha juhudi za wanafunzi wa masomo ya sayansi kwani wakati wa masika  walazimika kukosa  mafunzo ya vitendo  kwakuwa wananyeshewa na mvua wanapokuwa ndani ya maabara hiyo hivyo wameiomba serikali iwasaidie.
Kwaupande wake mmoja wa wajumbe  wa bodi ya shule hiyo michael sanga amekiri hali hiyo kuwa kikwazo  katika kuongeza ubora wa elimu na kuongeza kuwa serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni hasini za kufanya ukarabati wa baabara hiyo na sasa anatafitwa mkandarasi na  mkuu wa shule hiyo christopher malamsha amesema ukarabati huo utapokamilika ari ya wanafunzi katika  masomo ya sayansi itaongezeka.

0 comments:

Chapisha Maoni