Jumatatu, Aprili 17, 2017

ZIMBABWE SASA KULIPA MIFUGO SHULENI BADALA YA ADA

Serikali ya Zimbabwe imeruhusu wazazi kulipa ada kwa mifugo au kwa kufanya kazi ktk shule husika kama malipo.
Waziri wa Elimu ya Msingi na Sekondari, Dr. Lazarus Dokora amesema kwamba mamlaka za shule zinatakiwa kubadilika na kuacha kufukuza watoto kwa kuwa tu wazazi wao hawana pesa.
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dr. Sylvia Utete-Masango alifafanua kuwa mifugo itatumika kulipa kwa wazazi wa maeneo ya vijijini tu na mijini wazazi watalazimika kufanyakazi kama ujenzi kwenye shule husika endapo hawana pesa.
Zimbabwe inakabiliwa na uhaba wa pesa tangu mwaka jana baada ya Serikali kutishia kutaifisha makampuni yote ya kigeni nchini humo chini ya sheria ya kurudisha kila kitu kwa wazawa (Indigenisation and Empowerment Law).
Benki zililazimika kupunguza kiwango cha kutoa pesa hadi $40 kwa siku kwa kila mtu mmoja.

0 comments:

Chapisha Maoni