Jumamosi, Machi 25, 2017

VIDEO MPYA: LADY JAYDEE NA H_ART THE BAND KUTOKA KENYA WAMEKUJA NA 'ROSELLA'

Kwenye zile zinazotrend wekeend hii kutoka East Africa ni pamoja na hii ya H_Art The Band kutoka Kenya na Malkia wa Bongo Fleva Lady JayDee.
H_Art The Band kutoka Kenya na Lady JayDee wameshirikiana kutuletea wimbo wao mpya ‘Rosella’ ambayo video yake imeongoza na Kevin Bosco Jnr.
‘Rosella’ ni wimbo unaosimulia stori  ya mapenzi kati ya watu wawili waliobaki njia panda. Akiwa muoga wa kueleza hisia zake, Rosella anabaki kuumia akitamani yule ampendaye ajue kile kilichopo moyoni mwake, akiendelea kujiuliza kama kweli jamaa kabadilika… Lakini hata kama angekuwa na ujasiri wa kufanya hivyo, mwanaume huyo ana sababu zinazomfanya afikirie tofauti na pengine kujuta na kukata tamaa juu ya penzi hilo licha ya kuwa bado anampenda sana mrembo huyo.
Watazame na sikiliza stori za pande zote mbili kwenye hizi dakika tano hapa chini.

0 comments:

Chapisha Maoni