Jumatano, Machi 15, 2017

MAHAKAMA YA ULAYA ILIVYOHUKUMU VAZI LA HIJAB

Mahakama ya Haki ya Ulaya (ECJ) yenye makao yake huko Luxembourg jana Jumanne ilipasisha marufuku ya vazi la staha la mwanamke wa Kiislamu, hijabu.
Kwa mujibu wa hukumu ya mahakama hiyo, waajiri wa Ulaya wanaweza kuwazuia wafanyakazi wao kuvaa nembo za kidini likiwemo vazi staha la hijabu.
Hii ni hukumu ya kwanza kutolewa na mahakama ya Ulaya kuhusu mjadala wa vazi la staha la mwanamke wa Kiislamu, hijabu katika maeneo ya kazi. Mahakama ya Haki ya Ulaya iliyochunguza mafaili na matukio ya kufutwa kazi wanawake wawili wanaovaa vazi la hijabu katika nchi za Ubelgiji na Ufaransa imetangaza kuwa, ni haki ya kisheria ya kila shirika na kampuni kuwataka wafanyakazi wao kuwa na muonekano usioegamea upande wowote wala kuwa na alama za kidini, na mahakama hiyo imeruhusu mashirika kuzuia alama na nembo za kisiasa, kifalsafa au kidini.
Hukumu hiyo ya mahakama ya Ulaya ya ECJ kwa hakika imetolewa kwa shabaha ya kuzuia vazi la staha la wanawake wa Kiislamu, hijabu wanaofanyakazi katika makampuni na taasisi mbalimbali za Ulaya. Hatua hii si tu kwamba ni ubaguzi wa wazi dhidi ya wanawake wa Kiislamu, bali pia imewapa mamlaka makubwa waajiri kutumia hukumu hiyo kwa ajili ya kuwabana zaidi wafanyakazi wa kike Waislamu na kuwapa hiari ya ama kuvua mavazi yao ya hijabu au kufutwa kazi.

0 comments:

Chapisha Maoni