Alhamisi, Machi 30, 2017

BAADA YA KANDANDA, RONALDINHO SASA KATIKA MUZIKI, TRACK YAKE IKO HAPA +AUDIO

Staa wa soka na mkongwe wa Klabu ya Barcelona na Timu ya Taifa ya Brazil, Ronaldinho Gaucho ameamua kujitosa kwenye tasnia ya muziki ambapo ameachia wimbo wake wa kwanza alioupa jina la Sozinho.
Wimbo aliouachia Ronaldinho ni wa staili laini Kibrazili ya Samba na tafsri ya Sozinho kwa Kiingereza ni ‘Alone’
Hii sio mara ya kwanza kwa Gaucho kufanya kazi ya muziki, mwaka jana alipata nafasi ya kuimba kwenye mashindano ya Rio Paralympics 2016. 
Licha ya kuachia ngoma hiyo, Gaucho amesema: ‘Asanteni marafiki zangu. Huu ni wimbo wangu wa kwanza, bila kumshirikisha mtu yeyote!!!’
Licha ya kustaafu kucheza soka la ushindani mwaka 2015, Staa huyo wa Samba mwenye umri wa miaka 37 amekuwa akijishughulisha na kazi mbalimbali zikiwemo za muziki.

0 comments:

Chapisha Maoni