Jumapili, Septemba 14, 2014

YALIYOJIRI KATIKA MKUTANO MKUU WA CHADEMA

Mkutano mkuu wa Chama cha demokrasia na maendeleo Chadema, umeadhimia kuitisha na kuratibu,maandamano pamoja na migomo nchi nzima yasiyo kuwa na ukomo, ili kushinikiza kusitishwa mara moja kwa shughuli za bunge maalumu la katiba, linaloendela na vikao vyake mjini dodoma,na kuwagiza wanasheria wake wote, kuandaa mashtaka,kwa wabunge wote wanaoendelea na vikao vyao ndani ya bunge,kwa kufisadi fedha za walipa kodi watanzania.

Akitangaza maamuzi hayo jijini Dar-es-salaam,kwenye mkutano mkuu wa tano wa Chadema,mwenyekiti wake Mh  Freeman Aikaeli Mbowe,amesema jitihada za mazungumzo baina ya wao ukawa na viongozi wa juu wa serikali na chama tawala zimeonyesha kugongwa mwamba kwa shughuli za bunge kuendela na vikao vyake mjini Dodoma.
Aidha Mh Mbowe amesema kuwa ,chama cha demokrasi na maendelo Chadema, hakitamuonea haya kiongozi yeyote yule atakayejihusiha na vitendo vya rushwa au kutowajibika kwa wananchi na kuwa uongozi ni dhamana na hivyo kiongozi asiyewajibika kwa mujibu wa katiba atang’olewa hata kama muda wake wa uongozi haujakamilika kwa mujibu wa katiba.
Wakiongea kwenye mkutano huo viongozi wanaounda umoja wa katiba ya wanachi Ukawa,kutoka vyama vikuu vya upinzani nchini,CUF,NCCR-mageuzi pamoja na nld,ambapo kila mmoja kwa wakati wake wamesema kuwa ili kung'oa ccm madarakani ni kuunganisha nguvu ya pamoja kwa kumsimamisha mgombea moja ngazi ya urasi,na kuwa awali uoga na kutokuaminiana ndivyo vilikuwa vinawasumbua,ambavyo sasa havipo.
Msajuli wa vyama vya siasa nchini,Profesa Fransice Nutungi amewataka wanachadema kudumisha demokrasia waliyoinyesha wakati wa mchakato mzima wa uchaguzi ndani ya chama hicho,kuanzia ngazi ya chini hadi ngazi ya kitaifa na ndicho ambacho vyama vya siasa nchini vinatakiwa kutekeleza jukumu hilo la kikatiba ndani ya vyama vya siasa.
Mkutano huo uliohudhuriwa na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi,ambapo mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi ccm Dkt Jakaya Kikwete pamoja na uongozi wa juu wa chama tawala uliwakilishwa na makamu mwenyeikiti wa chama hicho tanzania bara bwana philip mangula,ambapo amesema kwenye siasa ni kushindana kwa hoja bila magonvi,yatakayopelekea uvunjifu wa amani iliyopo nchini.

0 comments:

Chapisha Maoni