Miaka 387 iliyopita katika siku kama ya leo, vilijiri vita vya mwisho
vya La Rochelle kati ya Wakatoliki na Waprotestanti wa Ufaransa. Vita
hivyo vilianza baada ya Waprotestanti kuchochewa na Uingereza.
Wakatoliki ambao walikuwa wakiungwa mkono na vikosi vya jeshi la
serikali ya Ufaransa chini ya uongozi wa Richelieu, Kansela mashuhuri wa
nchi hiyo, walipigana vita na Waprotestanti ambao walikuwa wakipigania
maeneo yao katika bandari ya La Rochelle. Vita hivyo vilimalizika baada
ya mwaka mmoja kwa kupata ushindi Wakatoliki na kutekwa La Rochelle.
Na miaka 154 iliyopita katika siku kama ya hii ya leo Paul Gottlieb Nipkow mmoja wa wavumbuzi wa televisheni alizaliwa huko Ujerumani. Nipkow alikulia katika familia maskini, lakini juhudi na irada kubwa ilimuwezesha kuendeleza masomo yake ya fizikia hadi chuo kikuu. Paul Gottlieb Nipkow alifanya utafiti mkubwa na hatimaye alifanikiwa kuvumbua transimita ya televisheni. Chombo hicho kilichobuniwa na Nipkow kiliweza kurusha mawimbi ya televisheni katika umbali wa mita 30 na baadaye transimita iliyotengenezwa na mvumbuzi huyo wa Kijerumani ilikamilishwa na wabunifu wengine.
Na miaka 154 iliyopita katika siku kama ya hii ya leo Paul Gottlieb Nipkow mmoja wa wavumbuzi wa televisheni alizaliwa huko Ujerumani. Nipkow alikulia katika familia maskini, lakini juhudi na irada kubwa ilimuwezesha kuendeleza masomo yake ya fizikia hadi chuo kikuu. Paul Gottlieb Nipkow alifanya utafiti mkubwa na hatimaye alifanikiwa kuvumbua transimita ya televisheni. Chombo hicho kilichobuniwa na Nipkow kiliweza kurusha mawimbi ya televisheni katika umbali wa mita 30 na baadaye transimita iliyotengenezwa na mvumbuzi huyo wa Kijerumani ilikamilishwa na wabunifu wengine.
0 comments:
Chapisha Maoni