Tarehe 31 Julai miaka 208 iliyopita ardhi ya Cape huko kusini mwa
bara la Afrika ilivamiwa na wanajeshi wa Uingereza. Ardhi ya Cape au mji
wa Cape Town ni sehemu ya kusini ya nchi ya Afrika Kusini iliyoko
pembeni ya Rasi ya Tumaini Jema au (Cape of Good Hope) ambayo ipo kati
ya bahari za Atlantic na Hindi. Eneo hilo lina utajiri mkubwa wa dhahabu
na almasi na ni kwa sababu hiyo ndiyo maana daima wakoloni wakawa
wanalikodolea jicho la tamaa.
Na siku kama ya leo miaka 70 iliyopita aliaga dunia Antoine de
Saint-Exupery mwandishi na mwanaanga wa Kifaransa katika Vita vya Pili
vya Dunia baada ya ndege yake kuanguka. Exupery alizaliwa mwaka 1900
katika mji wa Lyon nchini Ufaransa. Mwandishi Antoine de Saint Exupery
alijishughulisha na masuala ya kusafiri angani kutokana na kupenda sana
fani hiyo. Alijiunga na jeshi la Ufaransa katika Vita vya Pili vya Dunia
na kuwa afisa wa masuala ya usafirishaji wa posta. Siku hiyo Antoine de
Saint Exupery alirusha ndege hewani akiwa katika kazi zake za kawaida,
lakini ndege yake ilitoweka na mabaki ya mwili wake na ndege hiyo
hazijaonekana hadi leo hii. Mwandishi huyo ameandika vitabu kadhaa na
miongoni mwao ni "The Little Prince", "Southern Mail" na "Night Flight."
0 comments:
Chapisha Maoni