Alhamisi, Julai 31, 2014

KIKOSI CHA MBEYA CITY KUTANGAZWA WIKI IJAYO

Kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi amesema anatarajia kupata kikosi cha vijana 20 anaowahitaji kuanzia wiki ijayo ili kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Mchakato wa kutafuta vijana watakaocheza Ligi ya vijana, ulianza muda wa mwezi sasa, na amejipanga kutaja kikosi bora kitakachochanganyika na kikosi kikubwa katika maandalizi ya Ligi Kuu.

Akizungumza na Fichuo Tz Blog, Mwambusi alisema wiki hiyo pia wanategemea kutangaza kambi ya maandalizi, na kwamba uongozi wa klabu utaweka bayana kama watajificha wapi kujifua kwa kutengeneza kikosi hicho kiweze kuchukua ubingwa msimu ujao.
Tumeanza mchakato wa kupata timu bora ya vijana kwa muda mrefu kwa sababu nia yetu ni kuhakikisha tunashiriki Ligi ya vijana katika ushindani mkubwa, ili tuchukue makombe kote
alisema.
Mwambusi alisema msimu uliopita timu hiyo ya vijana haikufanya vizuri sana katika mashindano ya kombe la Uhai, pengine ni kwa sababu walikuwa ndio wanaanza kwa mara ya kwanza lakini sasa wataingia na makali kama timu kubwa.
Tumeona tuwe makini katika kuangalia kikosi chenye uwezo, ndio maana kuna ambao waliocheza mwaka jana wanaweza wasionekane msimu huu, tunaendelea kuangalia kwa kulinganisha viwango vyao
alisema.

0 comments:

Chapisha Maoni