Makao Makuu ya Kanisa Katoliki (Vatican), yametangaza kuwatambua
rasmi makasisi wake wanaoombea na kutoa pepo wanaowashikilia waumini
wao kama yanavyofanya makanisa ya Kipentekoste.
Uamuzi huo ambao ni wa kwanza kutolewa katika
historia ya kanisa hilo, umetolewa juzi na Papa Francis na kuchapishwa
kwenye gazeti la Vatican la L’Osservatore Romano.
Papa Francis (pichani) alibariki kundi la makasisi 250 kutoka nchi 30 ambalo huwaombea watu wenye pepo.
Alipoulizwa kuhusu uamuzi huo wa Papa, Makamu Rais
wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Severine
Niwemugizi, alisema taarifa hiyo siyo ya kushangaza kwa kuwa hata ndani
ya kanisa ipo ibada ya kuombea wagonjwa.
Alisema ingawa hakuisoma taarifa hiyo, anaamini
kwamba kwa kuwa kikundi hicho kimepewa idhini na Papa kinachotakiwa ni
kufuata taratibu za kanisa.
0 comments:
Chapisha Maoni