Jumapili, Julai 06, 2014

PAPA AMERUHUSU WANAMAOMBI KANISANI

Makao Makuu ya Kanisa Katoliki (Vatican), yametangaza kuwatambua rasmi makasisi wake wanaoombea na kutoa pepo wanaowashikilia waumini wao kama yanavyofanya makanisa ya Kipentekoste.
Uamuzi huo ambao ni wa kwanza kutolewa katika historia ya kanisa hilo, umetolewa juzi na Papa Francis na kuchapishwa kwenye gazeti la Vatican la L’Osservatore Romano.
Papa Francis (pichani) alibariki kundi la makasisi 250 kutoka nchi 30 ambalo huwaombea watu wenye pepo.
Alipoulizwa kuhusu uamuzi huo wa Papa, Makamu Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Severine Niwemugizi, alisema taarifa hiyo siyo ya kushangaza kwa kuwa hata ndani ya kanisa ipo ibada ya kuombea wagonjwa.
Alisema ingawa hakuisoma taarifa hiyo, anaamini kwamba kwa kuwa kikundi hicho kimepewa idhini na Papa kinachotakiwa ni kufuata taratibu za kanisa.

0 comments:

Chapisha Maoni