Wanasayansi wanasema kuwa wamefanya ugunduzi mkubwa
katika jitihada za kutibu ugonjwa wa Ukimwi kwa kulazimisha virusi
kuondoka katika maficho yao mwilini.
Virusi vya HIV huganda na kujificha katika DNA
ya mgonjwa na kuishi humo kwa miaka mingi bila ya kufanya chochote, hali
ambao inatatiza juhudi za kupata tiba.
Awamu ya kwanza ya utafiti huo
uliofanyiwa wagonjwa sita, ilionyesha kuwa matibabu ya chemotherapy
ambayo hupewa wagonjwa wa Saratani, kwa kiwango kidogo yanaweza kuamusha
virusi hivyo kutoka katika maficho yao.
Wataalamu wanasema matokeo haya ni ishara nzuri , lakini huenda isiwezekane kwa matibabau hayo kuangamiza virusi vya HIV kabisa.
Dawa za kupunguza makali ya HIV, zinaweza
kupunguza idadi ya virusi kwenye damu , maana kwamba waathiriwa wa HIV
wanaweza kuwa na maisha ya kawaida tu licha ya kuwa na virusi mwilini.
Lakini kuna tatizo moja hapa. Virusi vya HIV pia
vinaweza kugandisa DNA yake kwenye DNA ya binadamu, na hapo inakuwa
changamoto kwa matibabu kwani dawa haziwezi kivifikia.
Wakati mgonjwa anapoacha kutumia dawa zake, virusi hivyo huamka upya na kuanza kushambulia mwili.
Utafiti sasa unalenga kuangalia mbinu za kuondoa virusi hivyo kutoka katika maficho yao na kuviua.
0 comments:
Chapisha Maoni