Mwanamume mmoja katika jimbo la Kano, nchini Nigeria,
amepelekwa katika kituo cha matibabu ya kiakili baada ya kusema kuwa
hamwamini Mungu. Taarifa hii ni kwa mujibu wa shirika moja lisilo la kiserikali nchini Nigeria.
Mubarak Bala alizuiliwa kinyume na matakwa yake hospitalini baada ya familia yake kumpeleka huko kwa matibabu. Duru katika hospitali hiyo zimesema kuwa
mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 29 alitibiwa kwa matatizo ya kiakili
na kwamba hataendelea kuzuilikwa kwa muda mrefu.
Jimbo la Kano lina idadi kubwa ya waumini wa kiisilamu, na limekuwa chini ya sheria za kiisilamu tangu mwaka 2000.
Shirika hilo la kimataifa limesema kuwa wakati
ambapo Bala aliwaambia jamaa wake kuwa hamuamini Mungu, familia yake
uilimpekeka kwa daktari kuuliza ikiwa akili yake iko timamu.
Licha ya kufahamishwa kuwa mwanamume huyo hana
tatizo lolote la kiakili, familia ya Bala ilitafuta ushauri wa daktari
mwingine aliyewafahamisha kuwa hatua yake ya kumkana Mungu, inatokana na
matatizo ya kiakili.
Bwana Bala, ambaye ni mwanafunzi wa chuo kikuu,
alilazimishwa kupata ushauri wa daktari wa kiakili , ingawa alitumia
simu kuwasiliana na wanaharakati wa haki za kibinadamu.
Hospitali ambako alikuwa ana pokea matibabu
ilisema katika taarifa yake kuwa Bwana Bala hana tatizo lolote la
kiakili na kuwa yuko sawa.
Alilazwa hospitalini kwa sababu alihitaji kuchunguwa na daktari, ilisema taarifa ya hospitali hiyo.
0 comments:
Chapisha Maoni