Kutokana na tabia ya kuambukiza, magonjwa yanaweza kugawanywa
kimsingi katika makundi makuu mawili, yaani magonjwa yasiyoambukiza au
magonjwa yanayoambukiza.
Mkurugenzi na mtaalamu wa masuala ya elimu ya
maambukizi ya vimelea vya magonjwa na kinga ya mwili wa kituo cha
utabibu cha Chuo Kikuu cha New York, Dk Philip Tierno anasema asilimia
80 ya magonjwa yote ya kuambukiza husambazwa kwa njia ya kugusana moja
kwa moja na chanzo chenye vimelea vya ugonjwa au kwa kugusana na mtu
kupitia njia ya kushikana mikono.
Historia inaonyesha kuwa desturi ya kushikana
mikono ilianza zamani sana, yapata karne ya pili kabla ya kuzaliwa kwa
Kristo na makusudi yake yalikuwa ni kumthibitishia usalama mtu
unayekutana naye.
Katika jamii mbalimbali duniani, watu hushikana
mikono mara kwa mara kwa ajili ya kusalimiana, kupongezana, kupimana
nguvu, kusameheana na wengine kuonyeshana mshikamano wa kijamii.
Ingawa kushikana mikono ni jambo zuri katika
kuimarisha uhusiano wa kijamii, wanasayansi wa masuala ya afya ya jamii
wanaonyesha kuwa jambo hili pia linaweza kusababisha hatari za kiafya
hasa wakati wa mlipuko wa magonjwa hatari yanayosambaa haraka kwa njia
ya kugusana.
Dk Innocent Mosha wa Kitengo cha Uchunguzi wa
Magonjwa katika Hospitali ya Muhimbili anasema, vimelea vya maradhi
vinaweza kusambaa kwa urahisi kwa kupitia mikono yetu.
Kwa mfano anasema magonjwa yaenezwayo na virusi
kama mafua, husambaa kwa wepesi zaidi endapo watu watapeana mikono bila
kuzingatia kanuni za usafi. Pia anasema ugonjwa wa homa ya ini unaweza
kuambukizwa iwapo watu watashikana mikono, hasa ikiwa mmoja wao ana damu
yenye virusi vya homa hiyo au kuwa na michubuko na jeraha.
Magonjwa yanayosababishwa na vimelea vya maradhi huchangia kwa kiasi kikubwa maambukizi. Ni vyema watu wakazingatia usafi wa mikono, hasa baada ya kupenga kamasi, kupiga chafya, kutoka chooni, kabla na baada ya kulaanasema
0 comments:
Chapisha Maoni