Jumatano, Machi 05, 2014

WAPENZI WA MANCHESTER UNITED, HII NDIO KAULI YA MWISHO YA SIR ALEX FEGURSON KWA DAVID MOYES

Meneja wa zamani wa Manchester United,Sir Alex Ferguson anaamini David Moyes atakuwa na mafanikio makubwa klabuni hapo na angepaswa kupewa muda zaidi ili kuimarisha kikosi hicho cha Old Trafford.
Moyes amekuwa akijadiliwa sana kutokana na kazi aliyoifanya Man United tangu achukue nafasi ya Ferguson majira ya joto.
Man United ambao hawakucheza wikiendi iliyopita wakiwa nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi kuu ya Uingereza,wapo nyuma ya vinara Chelsea kwa pointi 18 na wanahali mbaya katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya mara baada ya kufungwa goli 2-0 na Olympiakos pale Athens,Ugiriki.
Kukosa kwenye michuano ya Ulaya kwa Man United ni kitu kitakachosikitisha sana kwa klabu hiyo ambayo alishatolewa kwenye kombe la FA na Swansea na kombe la Capital One na Sunderland ambayo ilifungwa fainali na Man City siku ya Jumapili huku mashetani wekundu wakitolewa mara zote hizo ndani ya dimba la Old Trafford.
Pia mabingwa hao watetezi wapo nyuma ya timu inayoshika nafasi ya nne,Manchester City kwa pointi 12 na wanahaha kutafuta tiketi ya kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya huku matumaini ya kutetea taji yakiwa yamefifia kabisa.
Ferguson  ambaye alikaanza kuinoa Man United mwaka 1986 nakusubiri mpaka mwaka 1990 kabla ya kupata taji lake la kwanza anahisi kuwa Moyes anaweza kupata mafanikio na anadhani anahitaji muda zaidi ili kuweza kuboresha timu na kuonyesha ubora wake.
Raia huyo ya Scotland alisisitiza kuwa,”Man United itakuwa sawa.Ni mapema sana na kumekuwa na mabadiliko makubwa.Moyes anahitaji muda.”
Ferguson aliongeza kuwa,”Nilikuwa pale kwa miaka 27,hivyo kuwa na meneja mpya,inachukua muda lakini watakuwa vizuri tu.

0 comments:

Chapisha Maoni