Rais Vladimir Putin wa Urusi amewaamuru wanajeshi wake waliohusika
katika luteka za kijeshi ambazo baadhi zikifanyika karibu na Ukraine
warudi kwenye kambi zao. Hayo ni kwa mujibu wa msemaji wake Dmitri
Peskov.
Luteka hizo zilizokuwa na lengo la kuonyesha utayarifu wa majeshi ya
Urusi, ni jambo lililozitia wasiwasi serikali za nchi za magharibi baada
ya Urusi kutuma mamiaya wanajeshi katika eneo lina Ukraine la Crimea
ambako wakaazi wake
wengi ni wenye asili ya urusi, ikiwa ni baada sya
kuangushwa rais wa zamani Viktor yanukovich na wapinzani wanaoelemea
upande wa magharibi.
“Luteka hizo zilizoanza wiki iliopita zitamalizika kama ilivyo pangwa,"hivyo ndivyo alivyoeleza msemaji huyo
Haikuweza kufahamika wazi ikiwa hatua hiyo ya rais Putin ni jaribio la
kuitekea baadhi ya wito wan chi za magharibi kuutuliza mzozo huo ambao
umeupa mtihani mkubwa mustakbali wa Ukraine .




0 comments:
Chapisha Maoni