Jumatatu, Machi 31, 2014

VIKOSI VYA AU VYAWAFYATULIA RISASI RAIA WA BANGUI

Wanajeshi wa Chad waliotumwa kulinda usalama wa raia katika Jamhuri ya Afrika ya Kati wamewafyatulia risasi raia huko Bangui mji mkuu wa nchi hiyo na kusababisha vifo vya raia wanane.
Bado haijafahamika nini kilisabababisha ufyatuaji risasi huo uliopelekea kujeruhiwa pia watu wengine kadhaa.

Baadhi ya ripoti zinasema kuwa idadi ya wahanga huwenda ikaongezeka.  Matukio yamekuwa yakijiri kati ya wanamgambo wa Kikristo wa Anti-Balaka na wanajeshi wa Chad huko Bangui.
Wanajeshi wa Chad ni sehemu ya kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika kilichotumwa huko Jamhuri ya Afrika ya Kati kusaidia kukomesha machafuko yanayoendelea sasa nchini humo kati ya jamii ya Waislamu na Wakristo yaliyoibuka mwaka uliopita.
Ikumbukwe kuwa Umoja wa Afrika umelitangaza kundi hilo la Kikristo kuwa ni la kigaidi.

0 comments:

Chapisha Maoni