Jumatatu, Machi 31, 2014

WAKIMBIZI WA KIAFRIKA WALALAMIKIA UBAGUZI ISRAEL

Wahamiaji wenye asili ya Afrika waliokimbilia katika ardhi za Palestina zilizopachikwa jina la Israel wamefanya maandamano kulalamikia ubaguzi wanaofanyiwa na viongozi wa utawala wa Kizayuni.
Wanaharakati wa haki za binadamu nao wameshiriki kwenye maandamano hayo kuwaunga mkono wakimbizi hao wa Kiafrika na kulaani siasa za kibaguzi za Israel dhidi ya wageni.
Itakumbukwa kuwa, mwaka jana bunge la Israel lilipitisha sheria iliyolalamikiwa sana ambayo imewapa ruhusa viongozi wa utawala wa Kizayuni kuwatia mbaroni wahamiaji wa Kiafrika na kuwaweka korokoroni kwa muda wa mwaka mzima bila ya kuwafikisha mahakamani.
Sheria hiyo imepitishwa na Wazayuni licha ya kwamba makumi ya maelfu ya wahajiri wanaofanya kazi huko Israel wanatoka katika nchi zenye migogoro kama vile Eritrea na Sudan Kusini.

0 comments:

Chapisha Maoni