Jumatatu, Machi 31, 2014

UCHAGUZI WA MABARAZA YA MIJI UMEFANYIKA UTURUKI

Uchaguzi wa mabaraza ya miji unafanyika leo nchini Uturuki, ambako zaidi ya wananchi milioni 50 waliotimiza masharti ya kupiga kura wanatarajiwa kupiga kura. 
Matokeo ya uchaguzi huo hasa katika miji ya Ankara na Istanbul yatadhihirisha nafasi ya kisiasa ya Waziri Mkuu Recep Tayyip Erdogan na mustakbali wa chama chake tawala cha AKP.
Chama cha Erdogan kinakabiliwa na ushindani mkubwa kutoka vyama vingine 6 vikubwa vya Uturuki vinavyoshiriki uchaguzi huo hasa chama cha upinzani cha CHP. Kwa miezi 10 iliyopita serikali ya Erdogan imekuwa ikikabiliwa na maandamano ya kupinga serikali, huku Waziri Mkuu huyo na wafuasi wa chama cha AKP wakikabiliwa na kashfa za ubadhirifu.

0 comments:

Chapisha Maoni