Jumatatu, Machi 31, 2014

EBORA YAZIDI KUITIKISA GUINEA

Kuthibitishwa kesi mpya za ugonjwa wa Ebola katika mji mkuu wa Guinea Conakry kumezidisha wasiwasi wa kusambaa virusi vya ugonjwa huo hatari nje ya mipaka ya nchi hiyo. 
Senegal jana ilifunga mipaka yake na Guinea ili kujaribu kuzuia kuenea Ebola, huku maafisa wa nchi jirani za Liberia na Sierra Leone wakifanya uchunguzi juu ya ugonjwa huo.

Watu 70 wamefariki dunia kutokana na ugonjwa huo nchini Guinea na wengine 111 wameambukizwa. Wizara ya Afya ya Guinea imetangaza kuwa, katika mji mjuu Conakry watu 8 wameambukiwa Maradhi hayo.
Shirika la Afya Duniani WHO limetangaza kuwa, mlipuko wa Ebola hivi sasa unahesabiwa kuwa mbaya zaidi tangu mwaka 2007 ambapo watu 187 walipoteza maisha kutokana na ugonja huo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Dalili za homa ya Ebola ni kuhara na kutapika sambamba na joto kali mwilini ambalo pia huandamana na uvujaji mkubwa wa damu. Homa ya Ebola huambukizwa kwa kugusa damu, jasho na kinyesi cha mtu mwenye virusi hivyo.

0 comments:

Chapisha Maoni