Jumatatu, Machi 31, 2014

WAJORDAN WAANDAMANA KUPINGA MPANGO WA WAMAREKANI

Wajordan wamefanya maandamano kupinga mpango wa usalama uliopendekezwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani John Kerry kuhusu Palestina.
Maandamano hayo yaliyofanyika mjini Amman, mji mkuu wa Jordan yamefanyika kupinga mpango huo wa usalama uliowasilishwa na Kerry kati ya Wapalestina na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel. Waandamanaji hao wameutaja mpango huo kuwa wenye lengo la kuangamizwa kabisa kadhia nzima ya Palestina. Aidha waandamanaji hao waliokuwa wameshikilia bendera za Palestina, walitangaza kuwa utukufu wa Palestina ni utukufu wa Jordan na kusisitiza juu ya hatari ya utawala huo bandia wa Kizayuni kwa nchi za eneo zima la Mashariki ya Kati. Wajordan hao waliokuwa wamejawa na hasira kali, walitoa nara dhidi ya Marekani na kuiunga mkono Qudsi na msikiti wa al-Qudsi Tukufu. Kwa mujibu wa mpango huo wa Marekani, karibu vitongoji vyote vya walowezi wa Kiyahudi katika Ukingo wa Mto Jordan, vitaendelea kuwa vya Wazayuni, huku karibu asilimia 80 ya maeneo muhimu yenye vitongoji hivyo yakitakiwa kukabidhiwa kwa utawala huo pandikizi wa Kizayuni.

0 comments:

Chapisha Maoni