Meneja wa Chelsea,Jose Mourinho ambaye timu yake ipo
kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya Uingereza anahisi kuwa Ubingwa wa
ligi kuu hiyo msimu huu upo mikononi mwa Manchester City.
Ushindi wa goli 3-1 dhidi Fulham katika mchezo wa wapinzani wa
magharibi ya London siku ya Jumamosi na kipigo cha Arsenal cha goli 1-0
kutoka kwa Stoke City kilifanya Chelsea kuongoza kwa tofauti ya pointi
nne huku Liverpool wakiwa katika nafasi ya pili.
Man City ambao walicheza fainali ya kombe la Capital One siku ya
Jumapili dhidi ya Sunderland na kufanikiwa kutwaa ubingwa wa kombe hilo
kwa ushindi wa goli 3-1 wapo katika nafasi ya nne wakiwa wameachwa
pointi sita.




0 comments:
Chapisha Maoni