Jumanne, Januari 21, 2014

KUTENGULIWA KWA IRAN, AIBU KUBWA GENEVA II

Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria Walid al Moallim amekosoa hatua ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ya kutengua mwaliko wake kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wa kushiriki katika mkutano wa Geneva II na kukitaja kitendo hicho kuwa ni kichekesho. 
Walid al Moallim ameashiria mchango mkubwa wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kuimarisha amani na usalama wa Mashariki ya Kati na kusema kuwa, si rahisi kupuuza nafasi ya Iran katika masuala ya usalama wa eneo hilo na kwamba ni kosa kubwa kutoalikwa Tehran katika mkutano wa Geneva 2. 
Amesema kuwa nchi ambazo hazitaki Iran ishiriki kwenye mkutano huo kwa hakika zinataka kuendelea hali ya sasa nchini Syria.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria amesema mwaliko wa Umoja wa Mataifa kwa Iran kushiriki mkutano wa Geneva 2 na baadaye kutenguliwa mwaliko huo ni fedheha ya kisiasa kwa taasisi hiyo ya kimataifa.
Mkutano wa Geneva II unaojadili suala la kukomesha mgogoro wa Syria umepangwa kuanza leo katika mji wa Montreux nchini Uswisi.

0 comments:

Chapisha Maoni