Jumanne, Januari 21, 2014

BUNGE LA SOMALIA LAPITISHA SERIKALI MPYA

Bunge la Somalia limepasisha kwa sauti nyingi serikali mpya iliyoundwa Ijumaa iliyopita na Waziri Mkuu wa nchi hiyo Abdiweli Sheikh Ahmed. Bunge hilo pia ambalo lilikutana jana mjini Mogadishu lilipasisha mipango ya serikali mpya ya Somalia katika kipindi cha miaka mitatu ijayo.
Wabunge hao walijadili siasa za serikali ya Abdiweli Sheikh Ahmed ikiwa ni pamoja na masuala yanayohusiana na usalama, uchumi, kuanzisha taasisi mpya za serikali na kukomboa maeneo ambayo yangali yanadhibitiwa na wapiganaji wa kundi la al Shabab.
Serikali iliyopasishwa jana na Bunge nchini Somalia ni ya pili baada ya kumalizika kipindi cha mpito Agosti mwaka 2012.  Mwezi Disemba mwaka jana Bunge la Somalia liliiuzulu serikali ya zamani ya nchi hiyo kwa tuhuma za kushindwa kutekeleza majukumu yake na hitilafu kali zilizokuwepo kati ya Waziri Mkuu na Rais wa nchi.
Serikali mpya ya Somalia itakuwa na jukumu la kutayarisha mazingira mazuri ya uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika mwaka 2016 na kushughulikia masuala mbalimbali ya ndani.

0 comments:

Chapisha Maoni