Jumatatu, Januari 20, 2014

KAGAME: NITAENDELEA KUSHIRIKIANA NA KENYA

Rais Paul Kagame wa Rwanda amesema leo kuwa nchi yake itaendelea kushirikiana na Kenya ili kulinda maslahi ya nchi mbili hizo.
Akihutubia Kongamano la Magavana wa Kenya katika mji wa Naivasha, Rais Kagame wa Rwanda amesema viongozi wa Afrika wanaweza kutatua matatizo yanayowakabili wananchi wao iwapo watawashirikisha katika hatua za kuchukua maamuzi badala ya kuchukua maamuzi ya upande mmoja. Rais Kagame ambaye alikuwa mgeni wa heshima kwenye kongamano hilo amewapongeza Wakenya kwa kukubali mfumo wa serikali za majimbo akisema ni kupitia mfumo kama huo ndipo huduma zinaweza kuwafikia kwa haraka. Amesema Rwanda imeona manufaa ya mfumo wa majimbo na angependa kuona hatua za maendeleo zinazoonekana nchini mwake ziweze pia kushuhudiwa nchini Kenya.
Hotuba ya Rais Uhuru Kenyatta imesomwa kwa niaba yake na Waziri wa Teknolojia  ya Habari na Mawasiliano, Dkt. Fred Matiangi ambaye amesema serikali ina azma na irada thabiti ya kuona mfumo wa ugatuzi unafanikiwa.

0 comments:

Chapisha Maoni