Jumatatu, Januari 20, 2014

DK. SLAA AKOSOA BARAZA LA MAWAZIRI

Siku moja baada ya serikali ya Tanzania kutangaza baraza Jipya la Mawaziri, wadau mbalimbali nchini humo wametoa maoni yao kuhusiana na baraza hilo.
Kambi ya upinzani hususan Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekosoa baraza hilo jipya kikisema Rais Jakaya Kikwete amewachezea shere Watanzania kwa kuwaondoa mawaziri wachapakazi na kuwabakisha wale wanaodaiwa kuwa ‘mzigo’. Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Wilbrod Slaa amesema baraza jipya la mawaziri linaashiria kushindwa Rais Kikwete kuelewa mahitaji ya Watanzania.
Wasomi kwa upande wao wamekosoa hatua ya Rais Kikwete ya kumbakisha Waziri wa Elimu, Shukuru Kawambwa, wakisema mwanasiasa huyo ameiletea Tanzania aibu kubwa baada ya wizara yake kukumbwa na kashfa mbalimbali katika miaka ya hivi karibuni. Baadhi ya mawaziri wamehamishwa kutoka wizara moja hadi nyengine huku baadhi ya manaibu mawaziri wakipandishwa vyeo na kuwa mawaziri kamili na mawaziri wengine wakipigwa kalamu nyekundu.   

0 comments:

Chapisha Maoni