Alhamisi, Desemba 12, 2013

SIKU KAMA YA LEO NDIPO REDIO ILIGUNDULIWA


Miaka 112 iliyopita sawa na tarehe 12 Disemba mwaka 1901, kwa mara ya kwanza katika historia ya mwanadamu, kulifanyika mawasiliano ya kwanza ya maneno kutoka eneo moja hadi eneo jingine huko Italia kupitia mawimbi ya radio na bila ya kutumiwa waya, hatua ambayo ilifungua ukurasa mpya katika sekta ya mawasiliano. Mbunifu wa transimita na chombo kilichotumika katika kuunganisha mawasiliano hayo alijulikana kwa jina la Gugliemo Marconi, mwanafizikia wa Italia. Baadaye Marconi alifanikiwa pia kuvumbua radio.

0 comments:

Chapisha Maoni