Alhamisi, Desemba 12, 2013

KENYA WAADHIMISHA MIAKA 50 YA UHURU

Leo ni Alkhamisi tarehe 9 Safar 1435 Hijria sawa na Disemba 12, 2012.
Siku kama hii ya leo miaka 50 iliyopita Kenya ilipata uhuru kutoka Uingereza.
Kenya ilivamiwa na kukaliwa kwa mabavu mwanzoni mwa karne ya 20 na mwaka 1920, nchi hiyo iliwekwa rasmi chini ya mkoloni Mwingereza.
Sambamba na kukoloniwa nchi hiyo, Wakenya walianzisha harakati ya wananchi ya kupigania uhuru na kujikomboa chini ya uongozi wa Jomo Kenyata.
Wazalendo wa Kenya walipata viti vingi vya uwakilishi katika Baraza la Kutunga Katiba katika uchaguzi uliofanyika mwezi Februari mwaka 1961.
Hatimaye Kenya ilijipatia uhuru katika siku kama hii ya leo na mwaka mmoja baadaye nchi hiyo ikaanzisha mfumo wa jamhuri chini ya uongozi wa Jomo Kenyatta.

0 comments:

Chapisha Maoni