
Timu 16 zitakazomenyana katika hatua ya mtoano ya mashindano ya
soka ya Klabu Bingwa barani Ulaya zilikamilika jana kwa mechi kadhaa
zilizofanyika katika viwanja tofauti.
Timu ya Barcelona na Uhispania ambayo ilikuwa tayari imejihakikishia
kushiriki awamu ya mtoano iliinyuka Seltic ya Scotland mabao 6 kwa
moja baada ya mshambuliaji machachari wa Barca Meymar kung'ara katika
mechi iliyochezwa uwanja wa Camp Nou. Neymar alipachika magoli matatu
kati ya sita na kuigaragaza Celtic.
Arsenal ya Uingereza imeingia pia katika raundi ya mtoano licha ya
kupigwa mabao mawili kwa nunge na Napoli ya Italia ikiwa ugegeni. Katika
kundi hilo The Gunners wameingia raundi ya pili kwa kuwa na pointi 12
nyuma ya Borussia Dortmund ya Ujerumani ambayo nayo ina pointi 12.
Bibi Kizee wa Torino, Juventus imeaga mashindano ya Klabu Bingwa
barani Ulaya baada ya kupigwa goli moja na Galatasaray ya Uturuki. Juve
ilihitaji kutoka sare ili iweze kuendelea na mashindano hayo lakini goli
la dakika ya 85 la mchezaji la Wesley Sneijder katika dimba la Türk
Telekom Arena mjini Istanbul limeua ndoto ya Juve na kocha wake Antonio
Conte.
AC Milan pia imefanikiwa kuingia raundi ya mtoano na kuwasitiri
Wataliano ambao timu zao mbili za Juve na Napoli ziliaga mashindano hayo
jana kwa kutoka sare ya bila ya kufungana na Ajax ya Uholanzi na
Chelsea imefanikiwa kusonga mbele kwa kuilaza Steaua Bucharest bao moja
kwa nunge.



0 comments:
Chapisha Maoni