Wakurugenzi watendaji kutoka nchi tofauti duniani leo
wanatarajiwa kukutana nchini Kenya katika mkutano unaofanyika kwa lengo
la kuwekwa mkakati wa kimataifa wa kukabiliana na jinai za mazingira.
Ripoti kutoka Nairobi zinaeleza kuwa, mkutano huo wa siku 3 umeandaliwa
na Mpango wa Mazingira wa Kimataifa kwa ushirikiano na Polisi ya
Kimataifa (Interpol) na mada kuu yake ni kuongezwa ushirikiano kati ya
taasisi mbalimbali na kuchukuliwa hatua za pamoja ili kukabiliana
kimataifa na jinai za kimazingira.
Taarifa ya pamoja iliyotolewa na waratibu wa mkutano huo hapo jana
imeeleza kuwa, Intepol na Mpango wa Mazingira wa Kimataifa zimefahamu
kuwa ushirikiano ndio njia pekee ya kufanikisha malengo ya taasisi na
mashirika mbalimbali ya maliasili, mazingira na viumbe hai na
kukabiliana na wanaovunja sheria za mazingira.



0 comments:
Chapisha Maoni