Jumatano, Novemba 06, 2013

MATUKIO MAKUBWA YANAYOKUMBUKWA DUNIANI LEO NOVEMBA 6

Siku kama ya leo miaka 1374 iliyopita yaani tarehe Pili Muharram mwaka 61 Hijria Imam Hussein AS mjukuu wa Mtume Muhammad (SAW) akiwa pamoja na familia yake waliwasili katika ardhi ya Karbala katika Iraq ya leo. Miezi kadhaa kabla ya hapo, Imam Hussein AS aliondoka katika mji wa Madina na kuelekea Makka akilalamikia utawala wa kimabavu wa Yazid bin Muawiya na baadaye akaelekea katika mji wa Kufa huko Iraq. Japokuwa watu wa Kufa mwanzoni waliunga mkono mapambano ya Imam Hussein na kumualika katika mji huo, lakini waliacha kumuunga mkono mjukuu huyo wa Mtume wa Uislamu kutokana na kuhofia utawala wa Yazid na vilevile ahadi nyingi za urongo za mtawala wa Kufa.

Tarehe 6 Novemba 1860 Abraham Lincoln aliyekuwa mpinzani wa utumwa nchini Marekani, alichukua madaraka na kuwa rais wa nchi hiyo. Katika kipindi cha uongozi wake vita kadhaa vilitokea nchini humo na kupelekea waliokuwa wakiunga mkono utumwa kushindwa. Abraham Lincoln aliuawa mwaka 1865 na mmoja wa wapinzani wa harakati za kupinga utumwa nchini Marekani.

Na siku kama ya leo miaka 35 iliyopita inayosadifiana na tarehe 15 Aban 1357 Hijria Shamsia, ulianza mgomo wa wafanyakazi wa Shirika la Redio na Televisheni ya Iran kwa lengo la kuushinikiza utawala wa Shah uondoke madarakani. Siku hiyo hiyo maafisa wa usalama wa Shah walivamia taasisi za magazeti na kuwakamata baadhi ya waandishi habari suala lililopelekea magazeti maarufu kusimamisha uchapishaji wake.

0 comments:

Chapisha Maoni