Jumatano, Novemba 06, 2013

ETHIOPIA KUKABILIANA NA AL SHABAAB

Serikali ya Ethiopia imeweka tayari askari wake wa usalama na polisi ili kukabiliana na mashambulizi yanayoweza kufanywa na kundi la as Shabab.
Taarifa rasmi ya serikali ya Addis Ababa imeeleza kuwa, wamepokea ushahidi kwamba kundi la as Shabab linaweza kushambulia nchi hiyo na kwa ajili hiyo askari wake wa usalama na polisi wameandaliwa kikamilifu.
Hayo yanajiri katika hali ambayo wiki 3 zilizopita Wasomali wawili waliokuwa wamejifunga mabomu walijilipua kati ya watazamaji wa mpira wa miguu wakati wa mechi kati ya Ethiopia na Nigeria. Kundi la as Shabab limesema kuwa, litashambulia nchi ya Ethiopia ili kulipiza kisasi cha kupelekwa wanajeshi wa nchi hiyo katika ardhi ya Somalia.

Vyombo vya usalama na upelelezi vya Ethiopia vimetangaza kuwa, kuna ushahidi unaoonesha kuwa, kundi la as Shabab linaungwa mkono na Eritrea ili kushambulia mji wa Addis Ababa na maeneo mengine ya Ethiopia.

0 comments:

Chapisha Maoni