Jumatano, Machi 30, 2016

UTAMADUNI WA AJABU: WASICHANA WANACHOMWA MATITI NA MAWE YA MOTO ILI KUONDOA HISIA ZA NGONO

Mamlaka nchini Uingereza zimebaini kwamba zaidi ya wasichana 1,000 ambao ni raia wa Uingereza wenye asili ya Afrika magharibi wanachomwa na jiwe lenye moto kwa matiti yao kama njia ya kuwazuia kupunguza hisia za kingono. 
Gazeti la Daily mail linasema wanaofanya vitendo hivyo wanatumia vifaa kama nyundo na mawe moto wakiamini itapunguza hamu ya mapenzi kwa wasichana na hivyo kuepusha mimba za mapema. 
Wanaamini pia matiti yao hayatakuwa makubwa na hivyo hayatavutia wanaume. 
Tamaduni hiyo ilitokea Cameroon ambako kila msichana mmoja kati ya wanne anaathirika.

0 comments:

Chapisha Maoni