Jumapili, Machi 27, 2016

JANJARUKA MWANAMKE! HII NI KUHUSU ELIMU, UMRI WA KUOLEWA NA KUZAA

Ambacho mabinti wanatakiwa kustuka , ni kwamba wengi wataolewa na bodaboda, wafanya biashara, ukibahatika mwanasiasa, kwa sababu wasomi hawana ajira, hivyo atakwambia nisubiri nipate kazi , utazeeka unamsubiri
Lakini pia kumbuka binti mzuri ni miaka 22,23,24,25.
Kwa mliofika chuo kikuu basi tufanye 26, 27na 28,
Ukifika 29 huwa ni mstari mwekundu hapa waweza angukia mikoni mwa mzee wa miaka 52.
Ni vizuri binti uzae miaka ya 20s na ukomo uwe 35 kwa maana ya kufunga kizazi na kuwaza maisha na kuanza kula ulivyoviandaa.
Ukivuka miaka 35 kwa mwanamke ujue umaskini hautoumaliza, yaani ununue nepi una miaka 40.
Vilevile afya yako itatengamaa.
Hivyo tunatakiwa kuzisoma nyakati
Ninyi wanaume umemaliza degree ya kwanza una miaka 26,27,28,na 29 kwa sasa bado unasema unajipanga huwezi kuoa sasa hivi.
Kumbuka dunia imeisha kulikuwa na ebora sasa nasikia VIRUSI VYA ZIKAA kwa akina mama na watoto, Leo mtu anakufa kwa kuanguka kama papai, huna mtoto historia ya marehemu huwa haichekeshi japo huzua walakini!!!
Kukaa unaenda nje na kutongoza tongoza bora oa tu ndugu.
Hakuna cku ambayo unaisubiri ujenge nyumba, uwe na gari maana wengi mnawaza kujenga kwanza, jenga na mkeo ili usimnyanyase.

0 comments:

Chapisha Maoni