Alhamisi, Januari 07, 2016

TAASISI ZA UMMA NDIO WADAIWA SUGU MKOANI MBEYA!!

SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC), Mkoa wa Mbeya linazidai taasisi za umma zaidi ya shilingi milioni 45 ikiwa ni malimbikizo ya malipo ya pango ya mwaka uliopita hali ambayo inadaiwa kukwamisha shughuli za shirika hilo.
Hayo yamesemwa na Meneja wa Shirika hilo Mkoa wa Mbeya ambaye pia anashughulikia Mkoa wa Njombe, Juma Kiaramba, mbele ya Waziri wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi, William Lukuvi alipotembelea shirika hilo ikiwa ni sehemu ya ziara yake mkoani hapa.
Kiaramba alizitaja taasisis zinazodaiwa na Shirika lake kuwa ni pamoja na Jeshi la Wananchi wa Tanzania ambalo linadaiwa kiasi cha shilingi milioni 30.5 na kwamba ndiyo taasisis inayodaiwa fedha nyingi kuliko zote.
Alizitaja taasisi zingine kuwa zinazodaiwa malimbikizo ya madeni hayo kuwa ni Ofisi ya Mwanasheria Mkuu ambayo inadaiwa shilingi milioni 9.9, Mkuu wa Polisi shilingi milion 1.5 pamoja na Hospitali ya kanda ya Rufaa Mbeya ambayo inadaiwa shilingi miloni 3.

0 comments:

Chapisha Maoni