Ijumaa, Januari 15, 2016

MWALIMU AJINYONGA RUVUMA, KISA??

Mwalimu wa Shule ya Msingi Peramiho, mkoani Ruvuma, Baraka Mwakajila, amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kutumia shati. 
Polisi walikuta barua sehemu aliyojinyongea iliyokuwa imeandikwa Januari 4 mwaka huu na mwanamke (jina linahifadhiwa), anayedaiwa kuwa ni mpenzi wake, ambaye alimtaka aachane naye na aendelee na maisha yake. 
Baada ya upekuzi zaidi, marehemu alikutwa na karatasi kwenye mfuko wa suruari, ambayo Mwakajila aliandika Januari 2, mwaka huu, akimtuhumu mpenzi wake huyo kuwa amekuwa malaya na mlevi.

0 comments:

Chapisha Maoni